Historia ya Mwanamakuka

Historia ya Mwanamakuka

cement

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2012
Posts
581
Reaction score
218
Nimekuwa nikisikia sana hili jina Mwanamakuka anasifiwa sana na baadhi ya redia kama nembo ya wanawake wajasiriamali. Binafsi nimetafuta google sijapata hints zozote!

Naomba mwenye kujua anifahamishe ni nani na mchango wape ni upi katika taifa hili maana nasikia sasa hivi kuna kuna tuzo zinaitwa jina lake.

mwanamakuka1.jpg

=========
Mwanamakuka kwanza ni mwanamke wa kwanza kabisa MJASIRIAMALI katika historia yetu.

Mwanamakuka alikuwa kipande cha mwanamke amepanda hewani,mlimbwende mwenye weusi wa sungusungu wenye mg'aro mithili ya chungu ndio ulikuwa ukimpa chati wakati ule.Alikuwa mcheshi mwenye cheko bashasha na mkarimu kwa watu.

DSCF2539.JPG

Hili ndilo eneo alilokuwa anaishi Mwanamakuka ambalo saivi limejengwa shule.

Alikuwa mnyamwezi wa Tabora ailiyekuwa akisafiri kufanya biashara na wakoloni ambao wakati huo walikuwa waarabu.Mwanamakuka alikuwa akisafiri kutoka Tabora mpaka bagamoyo kibiashara.Na hii ilikuwa karne ya 18 leo tupo karne ya 21 ni miaka mingapi iliyopita?

Ujasiriamali wa wakati huo ilikuwa ni mdadilishano wa mali ghafi,vyakula vya nafaka kama vile mahindi,mtama,uwele,pia vyungu,asali na chumvi.

Waarabu walikuwa wakimpa vyombo na bidhaa za kauri.Kama ujuavyo wakati ule biashara zilikuwa za kubadilishana zaidi.Mama huyu sifa yake inayomuweka katika historia ni ujasiriamali.

DSCF2535.JPG

Shule hii ilipewa jina lake (Mwanamakuka) kama ishara ya kumuenzi.

Mwanamakuka aliolewa na Chifu Pazi,chifu wa kizaramo.Walikaa katika ndoa na mumewe lakini hawakubahatika kupata mtoto kurithi na kuendeleza jina.

DSCF2600.JPG

Hiyo kama nyumba ndio kwa ndani kuna kaburi la Mwanamakuka na mume wake.

Alifariki mwaka 1793 na kuzikwa hapo Bagamoyo katika nyumba aliyokuwa akiishi na mumewe pia Chifu Pazi alifariki na kuzikwa hapo hapo.

DSCF2630.JPG

Kaburi la Mwanamakuka,lipo karibu sana na Pwani ya Bagamoyo.

Ili kuenzi kazi zake na mafanikio yake kwa wanawake kuna shindano linafanyika kila mwaka linaloitwa Mwanamakuka awards kama heshima ya kuenzi alichokifanya.

Habari zaidi...

HAKIKA HUYU MWANAMAKUKA ALIKUWA MWANAMKE WA SHOKA KATIKA ZAMA HIZO.
Mwanamakuka kwanza ni mwanamke wa kwanza kabisa mjasiliamali katika historia yetu.

Mwanamakuka alikuwa kipande cha mwanamke amepanda hewani, mlimbwende mwenye weusi wa sungusungu uzuri wake huo ndio ulikuwa ukimpa chati wakati ule, ukichanganyia
pia alikuwa mcheshi mwenye cheko bashasha na mkarimu kwa watu.

Alikuwa mnyamwezi wa Tabora ailiyekuwa akisafiri kufanya biashara na wakoloni ambao wakati huo walikuwa waarabu. Mwanamakuka alikuwa akisafiri kutoka Tabora mpaka bagamoyo kibiashara. Na hii ilikuwa karne ya 18.

Ujasiriamali wa wakati huo ilikuwa ni mbadilishano wa malighafi, vyakula vya nafaka kama vile mahindi, mtama, uwele, pia vyungu, asali na chumvi.

Waarabu walikuwa wakimpa vyombo na bidhaa za kauli, kama ujuavyo wakati ule biashara zilikuwa za kubadilishana zaidi. Mama huyu sifa yake inayomuweka katika historia ni ujasiriamali.

Mwanamakuka aliolewa na Chifu Pazi, chifu wa kizaramo. Walikaa katika ndoa na mumewe lakini hawakubahatika kupata mtoto kurithi na kuendeleza jina.

Alifariki mwaka 1793 na kuzikwa hapo Bagamoyo katika nyumba aliyokuwa akiishi na mumewe pia Chifu Pazi alifariki na kuzikwa hapo hapo.

Ili kuenzi kazi zake na mafanikio yake kwa wanawake kuna shindano linafanyika kila mwaka linaloitwa Mwanamakuka awards kama heshima ya kuenzi alichokifanya.
 
Some hints:

By Paul Owere
Her grave lies in the obscurity of the former slave shipping port of Bagamoyo; a place where, for centuries, thousands of Africans were shipped into slavery overseas. Very little is known about her being the first woman long-distance trader in Tanzania. Mwanamakuka ventured into barter trade as early as the 18th century when trade was a preserve for the male gender. Even in such adversity and stereotyping that characterized the pre-colonial Africa, the iron lady from Tabora dared to challenge the unknown trade.

According to documents, she exchanged traditionally made goods such as pots and other local artifacts with glassware and beads from the Far East. Her industriousness, coupled with the dazzling and exceptional beauty won the heart of Zaramo chief, Pazi, who took her hand in marriage.
 
kwa hiyo jina lake linachukuliwa kam role model kwa wajsirimali wanawake?! let's hope her bloodline wont's make a fuzz out of the idea... wakishajua wajanja wanabonda hela ya tukio...
 
Ok sio mbaya japo nahisi kuna kitu nyuma ya pazia kwa nn sasa hivi??
 
kwa hiyo jina lake linachukuliwa kam role model kwa wajsirimali wanawake?! let's hope her bloodline wont's make a fuzz out of the idea... wakishajua wajanja wanabonda hela ya tukio...


mkuu umenena kweli
 
huyo niliwahi kusikia jina anaitwa kibaka mmoja tandale kwa tumbo na alishakufa kwa kuchomwa moto
 
Ok sio mbaya japo nahisi kuna kitu nyuma ya pazia kwa nn sasa hivi??

Mjini hapa.. watu wakishanusa hela wanachakarika... huoni masemina ya WAMA kila kukicha yanatangazwa..... wanaweka kichwa kimoja cha ukweli toka sirikalini na wadhamini wanamwaga noti..
 
mhn! sina uhakika kama ni hivi sana lakini ninalokumbuka ni mmoja wa watumwa wa mwisho mwisho waliokombolewa wasiuzwe hili lilikuwa linampa umaarufu zaidi siku za nyuma sasa hili lingine mimi mgeni japo kiukweli sio kuwa nawabeza waliotoa tuzo hii lakini naungana na wenzangu kwa nini iwe sasa?
 
Ahsante mwanzoni nilipofika bagamoyo na kusikia jina hili LA Mwanamakuka lilinishinda kulitamka na nikajua ni kama majina mengine ya kina Bashite
 
Back
Top Bottom