Historia ya "Shikamoo"

Historia ya "Shikamoo"

mheshimiwamtemi

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2014
Posts
291
Reaction score
218
"Shikamoo" limekuwa ni neno linalotumika kuonesha heshima baina ya watu. Desturi na tamaduni za Afrika mashariki hutumia neno hili kama salamu ambapo anayeitikia husema "Marhaba".

Pengine umewahi kujiuliza mini hasa maana ya "Shikamoo" Binafsi nakumbuka kuna Mzee mmoja aliwahi kunitukana nilipomsalimia shikamoo cha ajabu hakuniambia sababu zaidi ya kusema "unajua maana yake?".

Ukoloni na utumwa ulitawala Afrika Mashariki tangy karne ya 8. Hapo awali maingiliano baina ya Waarabu na wenyeji wa upwa wa Afrika Mashariki yalikuwa ya kibiashara zaidi. Tangy biashara ya Utumwa ishamiri kuanzia Marne ya 14 na kuendelea wenyeji hao wenye miili mikubwa na nguvu walinunuliwa na kuuzwa ili wakatumike katika mashamba na shughuli mbalimbali za waarabu.

Wengi tunakumbuka jinsi biashara ya Utumwa ilivyokuwa haramu na dhariri. Masoko ya kuuza na kununua binadamu kama bidhaa zingine yalifunguliwa. Baadhi ya maeneo hayo ni Zanzibar na Bagamoyo ambapo watumwa walipelekwa kwa ajili ya kuuzwa.

Katika biashara hiyo ilikuwa ni kheri ya Utumwa aliyepata mteja wa kumnunua kuliko yule aliyekaa sokoni muda mrefu kwani alikuwa anateseka na kuteswa hali iliyowafanya wengine kupoteza maisha.

Hali ilikuwa hivi, wakati waarabu na wanunuzi kutoka middle east na far east walipofika sokoni ilimpasa mtumwa kujipogia deve yaani kushawishi ununuliwe. Kwakuwa watumwa hawakuruhusiwa kuongea maneno mengine basi iliwapasa kusema "Shikamoo" wakimaanisha mnunuzi ashike ndani ya mfuko wake wenye fedha ili amnunue... Baada ya kujua bei mnunuzi aliitikia "Marhaba" akimaanisha Mali haba yaani hakuna na kiasi kile cha fedha kutosha kumnunua Utumwa yule.. Basi Utumwa aliangua kilio.

Leo tunatumia kama salamu. Yapi ni maoni yako mdau wa JF? Tuendelee au kuache kusalimiana shikamoo?
 
Umetulisha matango pori hapo mi navyojua ile ilikua salamu ya watumwa wakimaanisha NIKO CHINI YA MIGUU YAKO labda kama tafsiri imebadilika sawa
 
Maneno yanatoholewa kutokana na msimu mengine hufa na mengine huendelea kuishi. Hiyo salama sasa humaanisha heshima ya mtu aliyembele yako. Ukishindwa vyote mwambie Mambo uone neno gani halina heshima.
 
Watu weusi walikuwa wajinga, washamba na Dhaifu sana tangu zamani.

Wamekuwa watumwa kwa wa races zingine ndani ya ardhi yao.

Kama hawakuwa na ubunifu wa kubuni na kutengeneza silaha walishindwa hata kutengeneza umoja wao (Unity) wafight dhidi ya utumwa na udhalilishaji

Hopeless kabisa.
 
Mh.... kama haijakolea vizuri... yaaani iko kwa mbaaaali.. hebu ongeza kidogo mkuu tunajua sukari haba ila ongeza ikoleeee.
 
Kwanza maana ya Shikamoo yamejulikana tangu zamani kabisa! (tazama kamusi ya Madan ya mwaka 1903: "Shikamuu (also shortened into Shikamu, Shikam, Kamu, and even Kara), a common salutation used by a slave, woman, or dependant, to a superior, i.e. * your humble servant.' In full, nashika miguu yako, I hold your feet,—as a sign of inferiority and submission.") Tangu miaka mingi watu walisema haifai tena leo hii. LAKINI kinyume ya mawazo haya matumizi ya salamu hiyo yamepanuka na kuzidi. Siku hizi ni watu wengi zaidi wanaoitumia kuliko miaka 20 iliyopita. Basi jinsi ilivyo katika kila lugha: maneno hubadilisha maana. Watu wanaoitumia hawajitazami tena kama "watumwa".

Pili tafsiri yako ya "marhaba" kabisa si kweli. "Marhaba" (مرحبا ) ni salamu ya kawaida ya Kiarabu iliyopokelewa katika lugha nyingi (Waturuki wanasema "merhaba"). Waarabu husalimiana "marhaba - marhaba", au "marhaba - marhabteen". Tafadhali fanya utafiti kabla ya kusambaza stori.

Tatu: historia yako si sawa. Jaribu kusoma vitabu kadhaa. (angalau pitilia wikipedia mfano East Africa - Wikipedia). Afrika ya Mashariki haikutawaliwa na utumwa na ukoloni tangu karme ya 8. Unachoeleza kuhusu biashara ya watumwa ina hitilafu nyingi pia.
 
Sina uhakika na tafsiri yako, ila all in all hii salam ni ya kikuda sana.
 
Salamu yoyote inatokana na mapokeo ya jamii kutumia neno flani Kama salamu na sio historia.

Mtoto Mdogo anapojua kuongea anakuta binadamu wenzie wanasalimia shikamoo naye atalichukua na kuendelea nalo sio kuangalia historia.

Yawezekana Ni kwako na wachache wanapotamka au kutamkiwa maneno wanaanza kwanza kufikiria historia ya neno au chimbuko la neno.

Wengi wetu tunaangalia maana inayoprevail kwenye jamii kwa wakati tuliopo sio uliopita.

Sasa usianze kuchimbua na historia ya salamu ya "Mambo" haisaidii kitu chochote

Tizama maana iliyopo wakati uliopo sio huo wakati ambao hukuwepo.
 
Ni kheri salamu yangu ya uheheni ya kamwene kuliko shikamoo. Ukitaka kujua kuwa salaam ya shikamoo ni ya kitumwa utagundua kuwa yenyewe huwa inaelekea upande mmoja mdogo kwenda mkubwa, ni salam ya kipuuzi haioneshi upendo, hata mkubwa anapaswa kumsalimu mtoto. Ni kheri salaam ya kamwene haina mwanzaji kuliko shikamoo! I really hate shikamoo. Hata watoto wangu siwafundishi wanisalimie shikamoo, ama waseme kamwene au amani iwe juu yako. Mimi pia nafanya hivyo kwao

Salaam ya shikamoo asili yake ni utumwa. Mwalimu Nyerere alipaswa kuchagua moja katika salaam za makabila kuwa salamu yetu. Heri salaam yetu ingebaki kuwa "salaam" na mtu akakujibu "salaam" au "Amani" na mtu akakujibu "amani"
 
Back
Top Bottom