Ukienda katika jamii zetu hata watoto wadogo ambao hawajui maisha yanaendaje wanaamini mzungu ni mtu bora kuliko mtu mweusi.
Nimejiuliza sana dhana hizi zinatokana na nini lakini nimekuja kubaini kuwa dhana hizi walitujengea wakoloni enzi za ukoloni.
waafrika walichukuliwa kama tabaka la chini kabisa katika jamii na waafrika wote walioshuhudia yaliyokuwa yakitendeka katika jamii waliamini hivyo kuwa mtu mweupe ni bora kuliko mweusi.
Sasa shida ikaja kwenye jamii zetu kutunga vitu vinaitwa historia na kuendeleza simulizi za yaliyotukia enzi hizo kwa watoto wadogo vizazi na vizazi. Watoto hawa mbali na kwamba hawakuwepo kushuhudia hayo, lakini hadithi za mababu zetu waliuzwa, waliteswa, walitumikishwa zinaishia kuwajengea picha za yaliyotukia enzi hizo na wao kuamini mtu mweupe ni bora kuliko mweusi.
ni sawa na baba aliyekuwa akipigwa na kuonewa na jirani yake na yeye kuwachukua watoto wadogo na kuwahadithia alivyokuwa akipigwa na jirani, hakika kwa akili za watoto za kupangana nani ana nguvu kuliko wote darasi na nani namba mbili, ukiwaambia nilikuwa nachapwa viboko na jirani basi wanamuona jirani kidume.
Historia ya kuwafundisha watoto ni ile inayowaonyesha jinsi babu zao walivyokuwa mashujaa ili kuwajengea kujiamini na wao kupambana.
watu wazima ndiyo pekee wasome historia zilizokuwa zikishusha utu wa watu wetu.
lengo ni kujenga jamii zetu zaidi badala ya kutumia madhira yaliyopita kuendelea kuharibu jamii zetu.
Nimejiuliza sana dhana hizi zinatokana na nini lakini nimekuja kubaini kuwa dhana hizi walitujengea wakoloni enzi za ukoloni.
waafrika walichukuliwa kama tabaka la chini kabisa katika jamii na waafrika wote walioshuhudia yaliyokuwa yakitendeka katika jamii waliamini hivyo kuwa mtu mweupe ni bora kuliko mweusi.
Sasa shida ikaja kwenye jamii zetu kutunga vitu vinaitwa historia na kuendeleza simulizi za yaliyotukia enzi hizo kwa watoto wadogo vizazi na vizazi. Watoto hawa mbali na kwamba hawakuwepo kushuhudia hayo, lakini hadithi za mababu zetu waliuzwa, waliteswa, walitumikishwa zinaishia kuwajengea picha za yaliyotukia enzi hizo na wao kuamini mtu mweupe ni bora kuliko mweusi.
ni sawa na baba aliyekuwa akipigwa na kuonewa na jirani yake na yeye kuwachukua watoto wadogo na kuwahadithia alivyokuwa akipigwa na jirani, hakika kwa akili za watoto za kupangana nani ana nguvu kuliko wote darasi na nani namba mbili, ukiwaambia nilikuwa nachapwa viboko na jirani basi wanamuona jirani kidume.
Historia ya kuwafundisha watoto ni ile inayowaonyesha jinsi babu zao walivyokuwa mashujaa ili kuwajengea kujiamini na wao kupambana.
watu wazima ndiyo pekee wasome historia zilizokuwa zikishusha utu wa watu wetu.
lengo ni kujenga jamii zetu zaidi badala ya kutumia madhira yaliyopita kuendelea kuharibu jamii zetu.