Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,761
- 216,011
Mihogo ni moja ya mazao makuu ya chakula katika nchi za ki tropic. Mihogo iligundulika kama mizizi inayofaa kwa chakula 900 BC huko Brazili na Bolivia. Wareno walitawala Brazil kwanza kabla ya kugundua Afrika. Enzi hizo katika usafiri wa meli walichukua wa Brazil wenye ujuzi ili kuwasaidia katika kazi za utawala Afrika. Wabrazili hawa walisafiri na mbegu zao za mihogo kuileta Afrika miaka ya 1850.
Mtwara na mikoa ya kusini mpaka Pwani mihogo inalimwa sana. Mtwara inapakana na Msumbiji, Msumbiji lilikua koloni la Wareno. Mihogo ni chakula chenye wanga kwa wingi. Wanga ni muhimu kwa mahitaji ya kila siku ya mwanadamu.
Wahenga wetu walijifunza kuihifadhi mihogo ili iwasaidie katika siku za njaa. Walimenya mihogo na kuianika . Mihogo iliyokauka huitwa makopa. Makopa yakitwangwa hutoa unga wa ugali., Makopa pia hupikwa na nazi kama kufungua kunywa.
Mihogo ni moja ya vyakula vikuu Brazil na hivi ndivyo wanavyoandaa.
Mtwara na mikoa ya kusini mpaka Pwani mihogo inalimwa sana. Mtwara inapakana na Msumbiji, Msumbiji lilikua koloni la Wareno. Mihogo ni chakula chenye wanga kwa wingi. Wanga ni muhimu kwa mahitaji ya kila siku ya mwanadamu.
Wahenga wetu walijifunza kuihifadhi mihogo ili iwasaidie katika siku za njaa. Walimenya mihogo na kuianika . Mihogo iliyokauka huitwa makopa. Makopa yakitwangwa hutoa unga wa ugali., Makopa pia hupikwa na nazi kama kufungua kunywa.
Mihogo ni moja ya vyakula vikuu Brazil na hivi ndivyo wanavyoandaa.