Hivi BOT na TCRA wako wapi hizi riba za mikopo ya Tigo na Airtel?

Beberu10

Member
Joined
Jun 1, 2017
Posts
10
Reaction score
5
Wanajukwaa habari, nimekuwa nikijiuliza, hizi taasisi za serikali mbona ziko kimya sana, wakati.ndizo.zenye jukumu la kumlinda mlaji wa mikopo hii ya kwenye simu kutoka tigo na airtel ambao kiukweli wanamwibia mteja. Tigo ukikopa shilingi 120,000/= kwa siku 21 unatakiwa urudishe shilingi 144,600/= ambayo hii ni sawa na riba ya 27.3% kwa mwezi au 328% kwa mwaka, jamani huu ni wizi, hata kama hii mikopo risk yake ipo juu.

Airtel wao ukikopa shilingi 136,000/= utatakiwa urudishe shilingi 161,092/= baada ya siku 21 ambayo ni sawa na riba ya 24.6% kwa mwezi au 320% kwa mwaka.

Kidogo afadhali ni voda ambao wao wanakopesha kwa mwezi, ukikopa shilingi 46,000/= utalipa shilingi 50,140/= baada ya mwezi mmoja, hii ni sawa na riba ya 9% kwa mwezi au 108% kwa mwaka. Japo hii iko juu ila ni nafuu ukilinganisha na mitandao mingine.

Kwa hili naomba BOT na TCRA waingilie kati kulinda haki ya mteja, badala ya kuyaacha haya makampuni ya simu yakiwaibia wateja

Nawasilisha.
 
Tusubiri tuone kama watalifanyia kazi
 
Uzuri wa hii mikopo ni kwamba huweki rehani chochote ,na pia huna haja ya kujieleza ili upatiwe mkopo,pia unaweza lipa kidogo kidogo,na hata ukichelewa kulipa kwa upande wa tigo huongeza riba mara moja tu na haingozewi tena mpaka utapo lipa.huu ni upande mwingine wa faida zake
 
Utaratibu wa kukopa kwa voda ukoje, sijawahi ona hiyo option/menu
 
Sema wanasaidia, Lakini Airtel Money ndo wezi , Mimi wananikopa laki saba lakini baada ya wiki tatu unarudisha riba 185,000 , VODA hao angalau lakini Mkopo wao ni pesa kidogo mimi wananikopesha mwisho laki nne,
 
Hahahaha kama nimekosa ASSIST sehemu nyingine nifanyaje zaidi ya kukopa mkuu
Ukikosa assist hata kwenye PM, hapo unakuwa huna cha kufanya. Unakopa kimyakimya kwa hao wanyonyaji... lakini sasa usilalamike maana umeyataka mwenyewe kwa shida zako...
 
Hizo riba za makampuni ya simu hazina tofauti na mikopo ya mitaani, riba yao inatisha na kuogofya.

Vv
 
Ukikosa assist hata kwenye PM, hapo unakuwa huna cha kufanya. Unakopa kimyakimya kwa hao wanyonyaji... lakini sasa usilalamike maana umeyataka mwenyewe kwa shida zako...
Hahaha sawa mkuu
 
Nilikopaga 7000 airtel nikakaa miezi 3 riba ikaja 32000
 
Ni kweli mkuu! Hizi ni unsecured loans so the risk is too high and when the risk is high, lenders will demand more interest to compensate for the risk...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…