Ngurubhe
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 1,840
- 1,049
Mimi naamini kuwa kuna wakati Watanzania tunatatizo la kutenganisha ushabiki wa kisiasa na ushabiki katika vitu vingine.
Pamoja na kuwa kuimba ni kipaji lakini ni zawadi toka kwa Mungu, na ndio maana sio kila mtu anaweza kuimba.lakini ni rahisi sana kusifia au kuponda kazi aliyoifanya mtu mwingne.
Sitaki kusema Diamond yupo sahihi kwa baadhi ya shutuma zinazo ongelewa kumhusu,laa hasha bali nataka kusema kuna wakati tunapaswa kujua Diamond ni mtanzania na amesimama kama mtanzania kuwaakilisha tulio wengi.kwa namna anavyoishi kimziki na hata maisha yake ya kawaida.
Kama anaimba na kucheza vizuri asifiwe na aambiwe aongeze bidii,kama anajiskia,na kuwa na dharau bado hii haitufanyi kumkana na kuona ati hatufai kama wengi tulivyojikuta tunamzomea na kisha kumfanya aonekane sikitu mbele ya watu.mbona hivyo vitu havihusiani na kazi yake.
Hayo ni maisha yake bnafsi na madhara yapo kwake mweneyewe na maisha yake ya kawaida.
Na dhana hii ya kumfanya Ali kiba aonekane ni msanii bora kuliko Diamond ibaki kuaminika hivyo!!! Kwasababu si dhambi,lakini si lazima lifanyike kwa kupitia Diamond...
Hapa ndipo ninapowalaumu watanzania kuwa mmeshindwa kutofautisha ushabiki wa kisiasa na ule wa kimziki!?,kwani Alikiba hawezi kusifiwa bila kumtaja Diamond,nadhani hapa kuna udhaifu kimantiki!!!
kwamba tunataka kuaminishwa kuwa huwezi kujua kipi bora kama huna cha kulinganisha nacho?..,lakin si mazingira yana sadifuna kusema kiasi kwamba hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kias hiki,kumzomea kumponda kwenye mitandao ya kijamiina hata kumkweza mmoja na kumshusha mwingne kwa sabab ya hira tu!.
Kwa maneno rahisi Anavyoimba Alikiba ni tofauti na anavyo imba Diamond na kila mmoja anamashabiki wake.Kwa mantiki hiyo hiyo si busara mashabiki wa Diamond kumzomea Alikiba na si busara pia mashabiki wa Alikiba kumzomea Diamond.mim binafs naweza kusema huo ni ushamba na hali ya kukosa mwelekeo kiushabiki.
Ni mtazamo tu kwani hili leo limemtokea Diamond,si ajabu kesho likatokea Alikiba.tutawaathiri vijana wetu kisaikolojia badala ya kutuburudisha kisasa na kujiajiri tutawafanya warudi kutukaba mitaani.
Naamini alichofanyiwa Diamond si halali na hata wakati anashangiliwa siku za nyuma Alikiba hajawahi kuzomewa,na hata hapa niseme haitakiwi azomewe!,bora kutomshangilia kuliko kuzomea msanii bila sabab maalum,kwani atakuja kujua tu kuwa kakosea mahala fulani hata asipozomewa!.
Asanten.
Pamoja na kuwa kuimba ni kipaji lakini ni zawadi toka kwa Mungu, na ndio maana sio kila mtu anaweza kuimba.lakini ni rahisi sana kusifia au kuponda kazi aliyoifanya mtu mwingne.
Sitaki kusema Diamond yupo sahihi kwa baadhi ya shutuma zinazo ongelewa kumhusu,laa hasha bali nataka kusema kuna wakati tunapaswa kujua Diamond ni mtanzania na amesimama kama mtanzania kuwaakilisha tulio wengi.kwa namna anavyoishi kimziki na hata maisha yake ya kawaida.
Kama anaimba na kucheza vizuri asifiwe na aambiwe aongeze bidii,kama anajiskia,na kuwa na dharau bado hii haitufanyi kumkana na kuona ati hatufai kama wengi tulivyojikuta tunamzomea na kisha kumfanya aonekane sikitu mbele ya watu.mbona hivyo vitu havihusiani na kazi yake.
Hayo ni maisha yake bnafsi na madhara yapo kwake mweneyewe na maisha yake ya kawaida.
Na dhana hii ya kumfanya Ali kiba aonekane ni msanii bora kuliko Diamond ibaki kuaminika hivyo!!! Kwasababu si dhambi,lakini si lazima lifanyike kwa kupitia Diamond...
Hapa ndipo ninapowalaumu watanzania kuwa mmeshindwa kutofautisha ushabiki wa kisiasa na ule wa kimziki!?,kwani Alikiba hawezi kusifiwa bila kumtaja Diamond,nadhani hapa kuna udhaifu kimantiki!!!
kwamba tunataka kuaminishwa kuwa huwezi kujua kipi bora kama huna cha kulinganisha nacho?..,lakin si mazingira yana sadifuna kusema kiasi kwamba hakuna haja ya kutumia nguvu nyingi kias hiki,kumzomea kumponda kwenye mitandao ya kijamiina hata kumkweza mmoja na kumshusha mwingne kwa sabab ya hira tu!.
Kwa maneno rahisi Anavyoimba Alikiba ni tofauti na anavyo imba Diamond na kila mmoja anamashabiki wake.Kwa mantiki hiyo hiyo si busara mashabiki wa Diamond kumzomea Alikiba na si busara pia mashabiki wa Alikiba kumzomea Diamond.mim binafs naweza kusema huo ni ushamba na hali ya kukosa mwelekeo kiushabiki.
Ni mtazamo tu kwani hili leo limemtokea Diamond,si ajabu kesho likatokea Alikiba.tutawaathiri vijana wetu kisaikolojia badala ya kutuburudisha kisasa na kujiajiri tutawafanya warudi kutukaba mitaani.
Naamini alichofanyiwa Diamond si halali na hata wakati anashangiliwa siku za nyuma Alikiba hajawahi kuzomewa,na hata hapa niseme haitakiwi azomewe!,bora kutomshangilia kuliko kuzomea msanii bila sabab maalum,kwani atakuja kujua tu kuwa kakosea mahala fulani hata asipozomewa!.
Asanten.