Hivi huko duniani hali ipo kama Tanzania

Hivi huko duniani hali ipo kama Tanzania

Kommando muuza madafu

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2022
Posts
3,216
Reaction score
7,254
Kuna hii Kero ambayo ipo maeneo Mengi nchini sijui wenzangu mliosafiri kwenye nchi za wenzetu kuna hali kama hiyo.

Kero hii ni za wamachinga, bodaboda, madereva wa tax, wapiga debe na maajenti wa mabasi. Leo nitaongelea madereva wa boda boda, wapiga debe na machinga kwenye mastendi ya mabasi.

Ni kweli vijana wamejiajiri katika hizo sekta na wanapata vipato vyao halali. Ni jambo jema na la kushukuru ila hili suala la kulazimisha watu kununua, kupanda au kuwapangia nauli watakavyo wao si jambo jema. Mfano, Leo nipo Msamvu stend, atakuja Machinga anauza nazi mwingine anauza mikate, miwani n.k anasema ununue kuikataa akakasirika. Ukigonganisha macho na Machinga hapa stendi anakuulizia kama unanunua bidhaa yake. Kuikataa anakukasirikia. Hii kitu ipo hata kwenye boda boda/bajaji, ukigonganisha naye macho tu anataka akupakie kwenye pikipiki/bajaji yake. Maajenti na wapiga debe nao ni hivyo hivyo. Ukigonganisha nao macho tu, shida.

Kimsingi hii ni Kero kwetu wasafiri/wapitaji kwa maana toka nitoe kwangu kuka stendi au kupita kituo cha Boda najua naenda wapi na kama ningekuwa na uhitaji wa boda au bajaji au hivyo vitu wanavyouza ningewaita na kununua au panda usafiri wao. Utakuta mtu anauza miwani ile ya watoto nawe upo busy na mambo yako anakupitishia usoni au anakugusa mgongoni ili akuuzie au anakuomesha na kukuita hadi uitikie kwa kile anachotaka huduma. Usipoitikia anaona umemdharau lakini utaitikia na kununua kila.kitu kwa kila mtu ili umridhishe aone hujamdharau?

Sijui wenzetu mliosafiri nje ya nchi kuna utaratibu kama huu wa kulazimishwa huduma pale tu unapogonganisha macho na watoa huduma? Please, wahusika ondoeni hii Kero kwetu.

20230914_095617.jpg
 
Umeandika point kubwa sana kaka.Chanzo cha yote haya ni siasa.Viongozi serikalini wanaona kama kuwaacha wapiga debe na wauza vitu stendi wawasumbue abiria ni njia ya kupunguza uhaba wa ajira.Wakianza kuwapiga stop wanahisi reactions za majobless zitakuwa kali hadi kuhatarisha ulaji wao huko serikalini.
 
Mfano mdogo rwanda hakuna mambo kama haya. Lkn mkuu kwa mfano kituo cha mabasi kama magufuli mbona sio sehem ya kuish unapita mara moja unaondoka zako? Machinga hawawezi kuwa kero kwa kiasi kikubwa sNa kwa mpita njia, kuhusu wapiga debe ukiuchuna hakuna mtu atakusumbua kingne mara nyingne ukiweza kata tiket kwa njia ya mtandaoo hutasumbuka kutafuta ofis za mabaai mkuu
 
Mfano mdogo rwanda hakuna mambo kama haya. Lkn mkuu kwa mfano kituo cha mabasi kama magufuli mbona sio sehem ya kuish unapita mara moja unaondoka zako? Machinga hawawezi kuwa kero kwa kiasi kikubwa sNa kwa mpita njia, kuhusu wapiga debe ukiuchuna hakuna mtu atakusumbua kingne mara nyingne ukiweza kata tiket kwa njia ya mtandaoo hutasumbuka kutafuta ofis za mabaai mkuu
Ni kweli mzee Madirisha tunapita huko mastendi ila hio kero ipo kila sehemu. Ukipita kituo cha boda mkiangaliana usoni tu, haooo wanaleta pikipiki hata 4 miguuni mwako wakitaka uzipande hizo.
 
Boda boda ukigonganisha nae macho tu vroooom kashawasha boda unaenda eeh?!!
 
Hata machinga ni kero ya miaka yote, hawa watu wanatandika vitu barabarani ili wauze, matokeo yake wanazuia wapita njia wengine, hii ni kudhurumu haki ya mtumiaji barabara. Kimsingi hii ni kero, na hawalipi kodi, wanahama hama, aikuuzia kitu cha hovyo ukirudi humpati, hatoi risiti, wala hana elimu na anacho kuuzia. Ilimradi tu wana siasa wanawaona wapiga kura wao bas ndo misuguano haiishi. itafutwe namna nyingine ya kuwasaidia hao low income group wafanye shughuli za kuwaingizia kipato pasipo kusababisha kero kwa watu hata mazingira.
 
Back
Top Bottom