Hivi huyu aliyenialika 'Krismasi' Kwake kama hataki niende si aseme tu kuliko kunipa haya 'Masharti' ya 'Kukomoana' na 'Kuvunjana Moyo' mapema?

Hivi huyu aliyenialika 'Krismasi' Kwake kama hataki niende si aseme tu kuliko kunipa haya 'Masharti' ya 'Kukomoana' na 'Kuvunjana Moyo' mapema?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"GENTAMYCINE karibu sana Kwangu Kesho uje kula Krismasi ila ukija utalazimika kunawa sehemu Tatu zilizotengwa, na ikiwezekana utaenda katika Chumba Maalum ukaoge upya na Sabuni Maalum kisha utumie Sanitizer na mwisho kabla hujakaribia ndani itakupasa utuonyeshe Cheti cha Kuchanjwa UVIKO-19 na siyo mara moja bali mara Mbili" amesema Rafiki yangu aliyenialika.

Sikia Wewe Rafiki yangu hilo Pilau lako lisikufanye ukanitesa na Kunihangaisha hivi na isitoshe Mimi GENTAMYCINE ni Masikini Jeuri na hapa tayari nimeshatenga Buku Jero langu la Pilau Biriani 'Gengeni' kwa Bi. Paka wa Tandale na Jero lingine nalihifadhi nitanunua 'Pepsi Bigi' yangu na Sikukuu yangu naamini itaenda vizuri tu.

Sipendi Manyanyaso na Kwako siji tena!!
 
Back
Top Bottom