Hivi huyu Mama huwa anaelewa anachokisoma Kithungu?

Hivi huyu Mama huwa anaelewa anachokisoma Kithungu?

Bobby

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2008
Posts
2,182
Reaction score
1,896
Nimevumilia nimeshindwa sasa nimeamua kusema very objectively ili wanaohusika ambao najua huwa wanapita huku wachukue hatua stahiki kutuondolewa kadhia hii kwani si kilema. Nimekuwa nakereka kweli nimuonapo huyu mama anaposoma hotuba za kithungu, hana vituo, anaongea kama yuko peke yake hadhira hana muda nayo kabisa, yuko speed kiasi anakosea hata maneno ya kawaida kabisa. Mwaka wa nane huu sasa hili halifanyiwi kazi wakati si kilema linarekebishika kirahisi kabisa. Mnaohusika mna mpango gani na hili? Ni sawa kwenu tukaendelea kudhalilishwa kwa jambo lililo ndani ya uwezo wetu? Mods itazameni post hii kwa upana wake msikurupuke na kuiondoa pasi na kuangalia mantiki yake. Ninaipenda nchi yangu kwa dhati kabisa ndio maana nimeliandika hili kwa nia ya kujenga si kubomoa.
 
Nimevulia nimeshindwa sasa nimeamua kusema very objectively ili wanaohusika ambao najua huwa wanapita huku wachukue hatua stahiki kutuondolewa kadhia hii kwani si kilema. Nimekuwa nakereka kweli nimuonapo huyu mama anaposoma hotuba za kithungu, hana vituo, anaongea kama yuko peke yake hadhira hana muda nayo kabisa, yuko speed kiasi anakosea hata maneno ya kawaida kabisa. Mwaka wa nane huu sasa hili halifanyiwi kazi wakati si kilema linarekebishika kirahisi kabisa. Mnaohusika mna mpango gani na hili? Ni sawa kwenu tukaendelea kudhalilishwa kwa jambo lililo ndani ya uwezo wetu? Mods itazameni post hii kwa upana wake msikurupuke na kuiondoa pasi na kuangalia mantiki yake. Ninaipenda nchi yangu kwa dhati kabisa ndio maana limeliandika hili kwa ni ya kujenga si kubomoa.

Sasa kama unaopenda nchi yako mbona hujafunguka?
 
Mama gani huyo?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kithungu si mchezo jamani

Tatizo si 'kizungu'...tatizo ni kulazimisha kizungu, hotuba ya kuandikwa unaweza ukaitoa kwa kiSwahili na wale wageni wako wakawa na kopi za kiIngereza! Kwa nini ulazimishe au ulazimishiwe lugha usiyoimudu na kuhadhirika mbele ya umati, tena wa high level!
 
Swali zuri. Najua atalijibu

Idimi ubaunsa wote huo unataka kutuambia hujui ni mama yupi huyu anazungumziwa? Mpita Njia pamoja na uzururaji wako wote hujui ni mama gani anazungumziwa?
 
yaani utadhani yuko anafundisha watoto wa chekechea jinsi ya kutamka silabi. ikifikaga hapo kwake mi huwa nabadilsha channel.
 
Idimi ubaunsa wote huo unataka kutuambia hujui ni mama yupi huyu anazungumziwa? Mpita Njia pamoja na uzururaji wako wote hujui ni mama gani anazungumziwa?

We acha tu ndugu. Ni vijimambo tu vya sie wengine, huwa tunachelewa kung'amua mafumbo
 
Mkuu hata hotuba za Kiswahili nazo huwa zamtatiza...
Nimeshasikiliza mara nyingi sana hotuba zake kwenye dhifa mbalimbali...
Nadhani kuna haja ya kuangalia tena ushiriki wa wake za marais wetu kwenye majukwaa ya kimataifa...
Hakuna sababu ya kulazimisha mambo kama mtu hana taaluma na uwezo wa kutosheleza...

Ni wazi ni Salma K.

Kwa kweli ni bora awe anatumia Kiswahili tu kwani hicho anakimudu vizuri sana.
 
Mkuu hata hotuba za Kiswahili nazo huwa zamtatiza...
Nimeshasikiliza mara nyingi sana hotuba zake kwenye dhifa mbalimbali...
Nadhani kuna haja ya kuangalia tena ushiriki wa wake za marais wetu kwenye majukwaa ya kimataifa...
Hakuna sababu ya kulazimisha mambo kama mtu hana taaluma na uwezo wa kutosheleza...

Thanks watu8 kwa kuliona hili, actually hapo nilipobold ndio msingi wa post hii. Miaka 8 down the road mambo yako vile vile je kuna haja ya kuendelea kudhalilika? Kwenye kiswahili she is much better lakini bado kuna tatizo yaani ni mambo mengi yanachangia, pose la ufirst lady halipo, confidence ina shida na mambo kama hayo kibao. Sometimes positions huwa zinashape watu lakini naona hapa shaping inachukua muda mrefu sana sijui ni kwanini.
 
Nimevumilia nimeshindwa sasa nimeamua kusema very objectively ili wanaohusika ambao najua huwa wanapita huku wachukue hatua stahiki kutuondolewa kadhia hii kwani si kilema. Nimekuwa nakereka kweli nimuonapo huyu mama anaposoma hotuba za kithungu, hana vituo, anaongea kama yuko peke yake hadhira hana muda nayo kabisa, yuko speed kiasi anakosea hata maneno ya kawaida kabisa. Mwaka wa nane huu sasa hili halifanyiwi kazi wakati si kilema linarekebishika kirahisi kabisa. Mnaohusika mna mpango gani na hili? Ni sawa kwenu tukaendelea kudhalilishwa kwa jambo lililo ndani ya uwezo wetu? Mods itazameni post hii kwa upana wake msikurupuke na kuiondoa pasi na kuangalia mantiki yake. Ninaipenda nchi yangu kwa dhati kabisa ndio maana nimeliandika hili kwa nia ya kujenga si kubomoa.

Mbona kwako kunabomoka? Kaeni vivyo hvyo , mtabaki na labda wenzenu wanaingia kwenye historia
 
Mbona kwako kunabomoka? Kaeni vivyo hvyo , mtabaki na labda wenzenu wanaingia kwenye historia

Jaribu kuwa objective na avoid kupersonalize hii kitu. Hakuna mtu ana shida na huyu mama in person. Tungekuwa na shida naye tungeanza tangu akiwa Muhimbili Primary because we knew her since then. Tatizo letu ni position aliyonayo ambayo bahati mbaya au nzuri si yake peke yake ila inatuwakilisha sisi wote whether we like it or not. Je tukae kimya kwa jambo linaloweza kufanyiwa kazi? Hatupingi wao kuingia kwenye historia lakini je wanaingiaje? Nia yetu waingie vizuri kwenye historia na si vibaya kama trend inavyoonesha kwa sasa.

Kwangu hakubomoki nashangaa umelitoa wapi hili, kwa ushauri wangu mdogo zipitie upya sources zako za habari huenda zinakufeed ndivyo sivyo. Suppose kungekuwa kunabomoka bado gharama ni mimi na familia yangu tu may be ndio tungeilipa. Bahati mbaya kunapobomoka kwa huyu mama kama ilivyo hali halisi kwa sasa si yeye pekee anayeilipa gharama sisi wote kama nchi tunailipa hiyo gharama. Yeye ni reflection yetu sisi sote hakuna atakayesema ni tatizo lake binafsi. Sasa kama hatuwezi kuirekebisha je ni makosa kuisema ili kuwaamsha wahusika wafanye kitu kama wapo tayari? Sina shaka nimeeleweka.
 
Back
Top Bottom