hivi inawezekana ama ni kwangu tu?

hahaha wewe usidanganyike...mapenzi ata siku moja hayaanzi kwa maudhi always full shangwe na macare ya kufa mtuu...just jaribu kukumbuka wen husband mlivyoaanza nae...siajabu ulijikuta wasema haya haya maneno. hivyo basi nenda kwa mume wako mbembeleze mtekenye mpe love za ukweli mwambie mkumbushie yale mambo mliokuwa mnafanya wakati ndio kwanza penzi limewaka moto and all will be well....linda ndoa...nothing good has ever come out of extra marital affairs!!!!
 
We uc jidanganye bna tulizana magonjwa mengi ooho shauri ako.?
 
Mpenzi, pole sana. Sio wewe peke yako, wengi tunapitiaga kipindi kama hicho. Unapojisikia kutothaminiwa nyumbani, unahisi kama hawakustahili. Inaelekea kero unazopata hukuwahi kupata, ndo maana hukuwahi kuthamini swaga za mitaani. Hao wapo tu, tena hukawii kukuta hilo libaba limetelekeza familia, linampiga mkewe na kumcheat.

Chukulia urafiki tu, usiutie moyoni. Kama uko dhaifu, kimbia na uepuke kukutana na huyu baba. Cha muhimu, ongea na mumeo. Kama humuogopi, muambie wazi the way unavyonifanyia inaanza kunifanya ni-observe ninavyotendewa na total strangers na sioni kama ni sawa. Lakini kama mnaogopana, lalamika tu na uchukue hatua za kinidhamu kwake.

Pole, angalia usiache mbachao kwa msala upitao.
 


Kwa maelezo ya kisa chako ninashawishika kwa aslimia 100 wewe ndio tatizo kwenye ndoa yako na si mumeo kwa maneno machache inaonekana HUJATULIA unahitaji KUPEPEWA.Unachokitafuta utakipata tu.
 
Ila huu ushuhuda wa huyu dada unapaswa kuwa fundisho to all men! Mwanamke wako akipata attention kwako, hata hawezi ku-notice vitu vidogo vidogo anavyokutana navyo! I bet sio mara ya kwanza huyu dada anakutana na player/actors, lakini angekuwa happy nyumbani wala mawazo yasingemfikisha huku! Shauri zenu eeeh!
 
Hilo ni tatizo na kwa ushaur wa bure kaa mbali koz utararuliwa vibaya hicho kidubwana chako hapo chini afu jamaa atabadilika hutoamini! Sisi wanaume ndivo tulivo ukitaka kitu tia mbwembwe sana mpaka kieleweke. Tulia na mumeo na ongea nae kuhusu kero zenu!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 

We jamaa una akili sana aisee! Umetisha

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Mh usidharau dafu embe tunda la msimu
 

Wanasikiaga basi! Wewe twanga Maji kwenye kinu tu. Nimefuatilia comment zao, saaana wanamshangaa huyo dada na wala hawaoni mapungufu ya mume. Imagine ingekuwa the other way around, yaani mke hamjali mume, lbd anamfanyia gubu ungesikia 'mke mpumbavu huaribu ndoa yake kwa matendo yake'

Back to u dada, kiatu chako hicho vumilia; epuka vishawishi na Jaribu kutafuta japo kauzuri kamoja ka mumeo then capitalize on that. Huyo other man atakuwa ameoa, na kama ndivyo; fikiria anavyomkosea mkewe ndipo ujue kuwa ni wale wale wanaomaltreat home na kutreat nyumba ndogo kama queens!
 
Yote katika yote,mume wa huyu dada nae ni wa hovyo.Hajui majukumu ya mume ni pamoja na kumjali mke.Huyu dada amevutiwa na huyo jamaa kwa sababu amepata asichokipata nyumbani.Sijui akirudi kutaka something else itakuaje!
 
Shosti kizuri daima kinakua cha mwenzio,na usisahau zimwi likujualo halikuli likakwisha, huyo jamaa analake jambo analo fukuzia kwako na kama anagekua kufunguliwa milango na kubebewa Handbag ni jambo la mana basi usingemkuta wewe,ondoa mawazo yako kwa huyo mzee usifisidi ndoa yako kwa mpita njia.

Kaa chini tafuta sababu ya wewe kutokuelewana na mumeo ili usawazishe, kwani ukiweza kumvulia nguo huyo ujue shosti utamvulia mpaka mbeba mkokote sababu na yeye pia anakubebea mizigo.....
 

Dah pole sana mdada! hebu rudi usome tena ushauri wa Mr Rocky
Haya na mie nakupigilia msumari tena wa moto.... pamoja na kwamba sipo kwenye ndoa ila naomba nikupe kaushauri kadogo... kuna msemo unasema "usione soo sema naye" huu msemo ni mzuri kwa maana ya kwamba uwe muwazi kwa mumeo, usimuogope wala kuona aibu... tafuta siku moja iliyona furaha na iliyotulia toka out na mumeo mfanyie vitu ambavyo anapendelea na vitakavyo mfurahisha. then after muelezee ni jinsi gani unapenda utendewe/ufanyiwe... huenda hata yeye hajui kama ukifanyiwa hivo unafurahi.. mwambie napenda uwe unanifanyia hivi na vile.. ila usimwambie vitu vilivyocomplicated...
Chonde chonde usithubutu kuisaliti ndoa yako kisa ma-care ya siku moja tena co siku bali masaa.... huyo mbaba ni fataki na alifanya hivo ili akupate, CHEZEYA FATAKI WEWE naona hujakutana na mafataki. mwisho wa siku akikupata ana-kudump kama takataka..... USITEME BIG G KWA KARANGA ZA KUONJESHA.... kwa style hiyo utachezewa na kila takayepita mbele yake!
 
Last edited by a moderator:


Kwa nini usimfanye mumeo afikie huko
Kwa nini usifikirie kubadilisha ndoa yako unafikiria kutoka nje ya ndoa
Kwa nini unamkaribisha mvamizi mdudu alaye nafaka katika ghala lako la mahindi
Unategemea huyo mdudu atakuwa na huruma na wewe wakati umemkaribisha
Kwa nini unataka kujiangusha kw amakusudi kwa wema wa siku moja na sifa za kijinga za siku moja za fisi anamsifia mwanakondoo kuwa amependeza na angependa aende nae porini akampe chakula
Jiepushe na jiweke mbali na huo wema wa fisi mwenye uchu na njaa ambaye yuko tayari kurarua kila kilicho mbele yake
Huwa tunapenda sana kutumia udhaifu kutafuta kile tukipendacho na huyo jamaa kashaona opportunity na lazima aitumie so kuwa makini sana
 

Inategemea na mtu amelelewaje huko alikotoka, anaweza akawa ametoka ktk familia ambayo baba ni kila kitu na yeye kwa kuwa baba yake alikuwa anamchukulia mama yake kama anavyokuchukulia wewe na maisha yalienda basi na yeye mtazamo wake utakuwa hivyo, kwahiyo kama tabia yake ilikuwa hivi hivi tangu mwanzo kabla hajakuoa basi naona huyu mtu ndivyo alivyo na huenda hajichanganyi na wadau wengine kuona namna wanavyoishi na partner wao au ukute hata tamthilia huwa haangalii kuona namna ya ku-handle kinadada kama kuwasifia kiana na vitu vingine vidogo vidogo ambavyo kwa mwanamke ni vikubwa na vyenye thamani. Nawasilisha hoja je kabla ya kukuoa alikuwa hivyo kama sasa?
 

Kuna watu ni professional wa ma-care na ndio maana kuna mabrothermen kibao mjini unakuta hana ela lakini linapokuja suala la ku-take care yupo vizuri, atamshika mkono wakiwa wanatembea, nywele ikiwa inakijitu kadogo atakatoa na mambo mengine kama hata kumbeba kumvusha mferejini lakini mwisho wa siku inapokuja suala la kuwa na serious relationship (marriage) utaona mkaka miguu inaingia tumboni (anagwaya). Lakini all in all kuna vijana wengine huwa wanadhani fedha, nyumba nzuri na maisha mazuri kwa ujumla ndio kila kitu kwa mwanake kumbe kuna vitu vingine vidogovidogo vinatakiwa kukolezea.
 
Pole sana, vp lakini unamjali mumeo kama unavyotaka akujali, unamfungulia mlango??unamsalimu vizuri??unafanya kipi kinachoonesha uhitaji wako wa upendo uutakao??
Unajua kwamba na huyo mzee kwa mkewe ni kama mmeo kwako??
Una watoto??unahisi utawatendea haki kwa kutembea nje ya ndoa??
Tulia na Mungu wako na mwombe yeye akurekebishie ndoa yako, na tenda matendo mema naye atatenda utakavyo
Amina
 

Hebu nijibu maswali haya;
- Jee unayajuwa mabaya ya huyu bwana mgeni? Naam unayajuwa ya Mr/
- Jee huyu bwana angekuwa alimasi kama unavyomuona jee wangapi anao waliovutwa na wema wake?
- Mr alipokuaproach mara ya kwanza unakumbuka mema aliyokufanyia, lakini kabadilika jee huyu yeye itakuwaje?
- Jee gharama aliyotumia huyu bwana kukuteka moyo inalingana kiasi gani na anayoendelea kutowa huyo Mr.
-Jee Mr nae akitokea mwanamke nae akiwa tayari kujidai mbele yake ana haki ya kuhisi kama wewe?

Mlani shetani kwani huyo katumwa na shetani basi.
 
Kuwa tu muwazi unataka mambo ya huyo mshikaji, jiulize hubby wako akijua itakuwaje?na kila akikuudhi unagawa mambo utagawa kwa wangapi? mfukuzie mbali huyo pepo kabla hayajakukuta ukajuta baadaye
 
Kwa mtazamo wangu tulie kuwa msimamo huenda anafanya hivyo kama kukujaribu na wewe unataka kunasa wanawake jaman acheni hizo tamaa zinawapeleka wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…