manshiroo asante sana kwa ufafanuzi wako na nimekupata
Ila naomba kabla hujaamua kutoka nje au kuupokea wema wa huyo baba aliyekuja kwako jiulize maswali mengi sana kichwani mwako. Kama uliweza kuapa kuwa hutomvulia mwanaume yeyote nguo zaidi ya mumeo nenda na kiapo chako na wala usikiache
Nilalokuambia usidanganyike huwezi jua huyo jamaa anataka nini kwako au ana matatizo gani kiasi cha kuamua kukufanyia hayo
Anaweza kwa vigezo vyako akawa mwanaume wa kukucare sana na kukupenda upendo wa dhati ila vile vile anaweza kuwa nyoka ndani ya ngozi yake
Jiulize na jihoji mara mia mia kabla ya kukuba,li kuanguka na kuusaliti utu wako
Na jingine hebu siku moja jifunge umuombe outing mumeo mwende nae mbali na hizi kelele za magari na watu mkae mahali upasuke kila lililo moyoni mwako na mweleze kwa utaratibu kuwa hili na hili haliko sawa na jishushe mwambie kama na wewe kuna sehem uko wrong anzeni upya kama wakati wa uchumba
Ikiwork out you have your husband kama sio hapo
sitakuwa na la kukushauri tena