Hivi inawezekana tukafanya uchaguzi bila dosari? Wakenya je tupo tayari kweli kwa demokrasia ya kihivyo

Hivi inawezekana tukafanya uchaguzi bila dosari? Wakenya je tupo tayari kweli kwa demokrasia ya kihivyo

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Hapa nawaza na kuwasilisha, mahakama ya Kenya imebatilisha matokeo ya uchaguzi kwa kile ilichokitaja kuwa ukiukwaji wa katiba na tume huru ya uchaguzi. Japo mahakama iliomba muda ili itoe maelezo kamili kuhusu ilivyofikia kwenye hayo maaamuzi, hivyo kwa kifupi hadi hapo hakuna anayejua nini sababu haswa za kufutwa kwa matokeo, sote tunasubiri kwa hamu taarifa kamili.

Ninachojiuliza, hivi inawezekana tukarudia uchaguzi na ufanyike mwanzo hadi mwisho bila dosari? Ama ndio tena tutajikuta kwenye hali hii hii baada ya siku sitini zijazo. Kama Wakenya tumejiandaa vipi, maana kampeni zimeanza, hivyo inamaana tutaburuzana kwa miezi miwili ijayo, ikumbukwe pia Raila naye ameanzisha mtiti dhidi ya tume, hivyo lazima patachimbika hadi awatolee nje viongozi wa tume kama alivyofanya kwa wale wa awali.

Vipi katiba inasema nini, ama inawezekana tukarudia chaguzi mpaka basi, maana kila ikitokea dosari tutarudi hapa. Binafsi nina furaha kwa kuona mahakama zetu zimedhihirisha kuwa huru, lakini nahisi sisi wenyewe hatupo tayari kwa demokrasia ya kiwango hicho.
 
Mutongoria, nimefurahi sana kuona uzi huu. Asee ni kama wakenya walikuwa wamekula kona kwenye jukwaa hili. Limevamiwa tangu juzi na watz na habari zao zisizokuwa na miguu wala mikono na ushabiki wao kwa mambo yasiyowahusu na wasiyoyafahamu. Uchaguzi na IEBC si shida shida ni watu wengine wanaodhani wao ndo Kenya, na Kenya ndo wao! No magathie ooguo tu, makiumaga!
 
Kuwa huru ni pale tu wapinzani wanaposhinda ?

- The world is CRAZY and full of WANAFIKI.

Anyway ngoja MABILIONEA na SONS OF TYCOONS wanaoimiliki Kenya, UHURUTO na RAILA ODINGA waoneshane UMWAMBA maana they have got WEALTH then what else wanachotaka zaidi ya POWER

- Wenzangu na mimi tusiojua hata kesho tutakula nini tuendelee kuwa MAZWAZWA
 
Mutongoria, nimefurahi sana kuona uzi huu. Asee ni kama wakenya walikuwa wamekula kona kwenye jukwaa hili. Limevamiwa tangu juzi na watz na habari zao zisizokuwa na miguu wala mikono na ushabiki wao kwa mambo yasiyowahusu na wasiyoyafahamu. Uchaguzi na IEBC si shida shida ni watu wengine wanaodhani wao ndo Kenya, na Kenya ndo wao! No magathie ooguo tu, makiumaga!
Waoga nyie, watanzania wamevamua jukwaa, wakenya wote mmekimbia na kujificha nyuma ya kabati [emoji38]
 
Demoktasia ni "anasa" yenye gharama kubwa sana. Uchaguzi uliopita mlipewa $24m na wafadhili, zote hizo zimekaangwa tayari. Sasa mtafute nyingine, na labda nyingine zaidi kama sarakari hizi za kesi zitajirudia tena.
 
Mutongoria, nimefurahi sana kuona uzi huu. Asee ni kama wakenya walikuwa wamekula kona kwenye jukwaa hili. Limevamiwa tangu juzi na watz na habari zao zisizokuwa na miguu wala mikono na ushabiki wao kwa mambo yasiyowahusu na wasiyoyafahamu. Uchaguzi na IEBC si shida shida ni watu wengine wanaodhani wao ndo Kenya, na Kenya ndo wao! No magathie ooguo tu, makiumaga!

Kweli kabisa, kuna wapuuzi wamevamia humu na kuleta mada za kijinga na kitoto. Ngoja upepo wa uchaguzi upite waumini wa Jukwaa hili turudi.
 
Uchaguzi wa Kenya utakosa dosari pale tu mtakapofanikiwa kuondoa nafasi ya Ukabila katika uongozi.

Demokrasia inawapa watu uhuru wa kuchagua viongozi wao kwa vigezo vya kila aina, kwa mfano Tanzania huwa mnachaguana kwa vigezo vya uchama, unakuta Mtanzania hata umlishe nini hawezi akabadilisha chama, akiamka, akiota, akila, akinywa anawaza chama, kwake chama fulani ndio mwanzo mwisho wa akili na mawazo yake hata kama kikiwa na dosari za kivipi.
Hizo ndio athari za demokrasia, kwamba unachagua kigezo unachotaka kutumia kwenye kupiga kura. Na pia naona ukanda na ukabila umeanza kuwaingia nyie, leo hii wale wa kanda ziwa wanaimba sifa kweli kweli na huwaambii kitu.

Kenya viyo hivyo, sisi tumerogewa ukabila na sioni matumaini, japo kuna idadi kubwa ya Wakenya walio katikati (neutral) walimchagua aidha Raila au Uhuru kwa ajili ya sera. Kwa kifupi Raila, Kalonzo na Uhuru/Ruto wanatoka kwa kabila nne tu, hivyo Wakenya wengine wote walichagua bila kuzingatia ukabila.
 
How magnitude is that " Dosari" ? Nazani Hilo ndo swali la msingi, Kama hiyo dosari inaweza pelekea matokeo yakawa otherwise Kwamba badala ya jibu kuwa X likawa Y dosari hiyo haipaswi kuwa ignored Hata kidogo!
 
Demokrasia inawapa watu uhuru wa kuchagua viongozi wao kwa vigezo vya kila aina, kwa mfano Tanzania huwa mnachaguana kwa vigezo vya uchama, unakuta Mtanzania hata umlishe nini hawezi akabadilisha chama, akiamka, akiota, akila, akinywa anawaza chama, kwake chama fulani ndio mwanzo mwisho wa akili na mawazo yake hata kama kikiwa na dosari za kivipi.
Hizo ndio adhari za demokrasia, kwamba unachagua kigezo unachotaka kutumia kwenye kupiga kura. Na pia naona ukanda na ukabila umeanza kuwaingia nyie, leo hii wale wa kanda ziwa wanaimba sifa kweli kweli na huwaambii kitu.

Kenya viyo hivyo, sisi tumerogewa ukabila na sioni matumaini, japo kuna idadi kubwa ya Wakenya walio katikati (neutral) walimchagua aidha Raila au Uhuru kwa ajili ya sera.
sijawahi kukuona ukizungumzia jambo lolote la maana
 
Waoga nyie, watanzania wamevamua jukwaa wakenya wote mmekibia na kujificha nyuma ya kabati [emoji38]
Tulikimbia tukajificha mbali na uboya wa mijadala yenu jombaa, siunatujua sisi wakenya?Tunakuwaga na allergy ya ujinga!😀
 
Tulikimbia tukajificha mbali na uboya wa mijadala yenu jombaa, siunatujua sisi wakenya?Tunakuwaga na allergy ya ujinga!😀
Sawa bwana, waswahili wanasema akufukuzae hakwambi toka. Ujumbe tumepata.
 
Hizo arguments unazoleta hapa nadhani zilipelekwa tayari mbele ya majaji ila wakaamua uchaguzi urudiwe. kwa nini? waliona kasoro zilizojitokeza zilikuwa kubwa mno kuzipuuza na ziliathiri matokeo ya urais pakubwa
 
Demokrasia inawapa watu uhuru wa kuchagua viongozi wao kwa vigezo vya kila aina, kwa mfano Tanzania huwa mnachaguana kwa vigezo vya uchama, unakuta Mtanzania hata umlishe nini hawezi akabadilisha chama, akiamka, akiota, akila, akinywa anawaza chama, kwake chama fulani ndio mwanzo mwisho wa akili na mawazo yake hata kama kikiwa na dosari za kivipi.
Hizo ndio athari za demokrasia, kwamba unachagua kigezo unachotaka kutumia kwenye kupiga kura. Na pia naona ukanda na ukabila umeanza kuwaingia nyie, leo hii wale wa kanda ziwa wanaimba sifa kweli kweli na huwaambii kitu.

Kenya viyo hivyo, sisi tumerogewa ukabila na sioni matumaini, japo kuna idadi kubwa ya Wakenya walio katikati (neutral) walimchagua aidha Raila au Uhuru kwa ajili ya sera. Kwa kifupi Raila, Kalonzo na Uhuru/Ruto wanatoka kwa kabila nne tu, hivyo Wakenya wengine wote walichagua bila kuzingatia ukabila.

Huu ujumbe hauna mantiki, kwani watanzania wote (zadi ya milioni 50) wana jihusisha na vyama? Mbona ni wachache sana ndio wako kwenye vyama. CCM na ukubwa wake wote huo ina wanachama million 8, vyama vingine ni kidogo zaidi ya CCM. Daftari la wapigakuwa wa 2015 liliandikisha wapiga kura millioni 17, sioni kama ni kweli kama kila mtanzania ni shabiki wa chama fulani. Na hata kama mtu ni shabiki na habadili chama kunashida gani hapo? siasa si maamuzi ya mtu binafsi.
 
Sawa bwana, waswahili wanasema akufukuzae hakwambi toka. Ujumbe tumepata.
We si ni mwenyeji? Ujumbe hukuwa umelengwa kwako, pass it over, kwa hao mazombie walokuwa wamevamia hili jukwaa tangia juzi. Comment zao ziko hapa, we zisome, usije ukasema nipimwe mkojo! Big up kwako, your arguments are always refreshing! Huwa sitambui uraia wa mtu, kila ng'ombe na nundu zake!
 
waache hawa wabongo...jamaa wanashabikia jambo utadhani yesu amerudi...mbona hizi mammbo za kawaida tu? wapo mbali sana mkuu
 
Back
Top Bottom