Hivi jamani kwa nini hawa BRELA hawako makini katika kazi?

Hivi jamani kwa nini hawa BRELA hawako makini katika kazi?

Michael Amon

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2008
Posts
8,768
Reaction score
3,622
Kwa kweli hawa BRELA wameniudhi sana kwa kutokuwa makini katika kusajili majina ya biashara. Mnamo tarehe 6 december mwaka jana nilienda katika ofisi zao ili kusajili jina langu la biashara na mara baada ya kusajili nililipia malipo na kupewa risiti na kuambiwa nije nifuatilie certificate of registration.

Kutokana na shughuli nyingi na kuzungusha pale katika ofisi zao kuwa certificate of registration bado haijakamilika niliamua kurudi zangu nyumbani na kumwachia ndugu yangu mmoja anisaidie kufuatilia hizo certificate of registration.

Siku si nyingi huyo ndugu yangu alifanikiwa kuzipata hizo certificate of registration na juzi ndio amenitumia.

Lakini cha kushangaza baada ya kupokea certificate hizo jina la biashara lililoandikwa hapo ni tofauti na lile nililolisajili. Hivi jamani kweli huu ni uungwana? Mnashindwa kuwa makini hata katika vitu vya msingi kama hivi?

Siku nikienda dar nitaenda kupambana nao na lazima watanirekebishia tu.
 
pole sana ucsahau tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele tumia hilo hilo walokupa mkuu awawezi kubadili tena
 
Watanzania waliokuwa makini japo kidogo tu, hawaajiriwi, wanaajiri. Usishangae kwa hilo, hata huyo nduguyo uliyemwachia afatilie hakuwa makini kupokea nyaraka zenye jina ambalo silo.

Mimi yalinikuta nilipo renew passport yangu badala ya Faiza wakaandika Faizal na hata humu JF kuna mtu huniita Faizal badala ya Faiza nadhani ndio huyo huyo aliyeandika PP yangu. Niligoma kuichukuwa, ikabidi wanicheleweshe wiki.
 
Watanzania waliokuwa makini japo kidogo tu, hawaajiriwi, wanaajiri. Usishangae kwa hilo, hata huyo nduguyo uliyemwachia afatilie hakuwa makini kupokea nyaraka zenye jina ambalo silo.

Mimi yalinikuta nilipo renew passport yangu badala ya Faiza wakaandika Faizal na hata humu JF kuna mtu huniita Faizal badala ya Faiza nadhani ndio huyo huyo aliyeandika PP yangu. Niligoma kuichukuwa, ikabidi wanicheleweshe wiki.

You have a point FF.
 
Watanzania waliokuwa makini japo kidogo tu, hawaajiriwi, wanaajiri. Usishangae kwa hilo, hata huyo nduguyo uliyemwachia afatilie hakuwa makini kupokea nyaraka zenye jina ambalo silo.

Mimi yalinikuta nilipo renew passport yangu badala ya Faiza wakaandika Faizal na hata humu JF kuna mtu huniita Faizal badala ya Faiza nadhani ndio huyo huyo aliyeandika PP yangu. Niligoma kuichukuwa, ikabidi wanicheleweshe wiki.

Watu wako kusubiri mshahara wengi performance ziko chini ya kiwango
 
walikosea sarufi au muundo? kwa mfano waliandika "YOUNG MASTER HAIR AND BEAUTY SALON" badala ya "YOUNG MISTER HAIR AND BEAUTY SALOON"
 
Watanzania waliokuwa makini japo kidogo tu, hawaajiriwi, wanaajiri. Usishangae kwa hilo, hata huyo nduguyo uliyemwachia afatilie hakuwa makini kupokea nyaraka zenye jina ambalo silo.

Mimi yalinikuta nilipo renew passport yangu badala ya Faiza wakaandika Faizal na hata humu JF kuna mtu huniita Faizal badala ya Faiza nadhani ndio huyo huyo aliyeandika PP yangu. Niligoma kuichukuwa, ikabidi wanicheleweshe wiki.

Huu niuzembe uliopea. Sio siriwanastahili adhabu. We ngoja nikienda Dar naenda kuwasha moto BRELA. Mtaniona kwenye vyombo vya habari.
 
walikosea sarufi na jina la biashara halikukamilika
 
Back
Top Bottom