Inashangaza watu mnakurupuka na kuanza kumponda jamaa, yeye kama kasema maproducer wa kule wanamuhitaji tatizo liko wapi mpaka povu liwatoke? Marekani kuna maproducer wengi sana na wengine hata bongo hamuwajui kama kati yenu ni wanunuzi wa album za USA mtakuwa mashaidi wangu. Mfano Album ya mwisho ya Ice Cube kuna maproducer kibao ambao huwezi hata kuwajua lakini wameipika album ikaiva sasa Joh Makini kusema maproducer wa marekani wanamuita tafadhari wekeni mapovu pembeni na mtoe hoja zenye mashiko.