Ni ngumu kidogo kama umewahi kuwatizama wote katika vipindi vyao.
Wengi watasema Ronaldo de Lima kwa kuwa kizazi hiki kilimtazama na kumuona.
Wengi watasema Ronaldo kwa kuwa alicheza zama ambazo fursa ya kuangalia mpira ilikuwa kwa watu wengi zaidi.
Nimemuona Romario wakati wa Fainali ya kombe la Dunia mwaka 1994 USA.
Nimemuona Romario wakati wa kombe la America kusini miaka ya 1992 -1997.
Romario ni mchezaji namba tano katika orodha ya wachezaji wa karne huku Ronaldo akishika namba saba katika orodha hiyo.
Nimemuona Ronaldo akiwa na Brazil na kuiongoza kutwaa kombe la dunia. Nilimuona Ronaldo akitwaa tunzo kadhaa barani Ulaya na Duniani.
Ni ngumu kuwalinganisha miamba hawa lakini kwangu Romario De Souza anazidi kidogo.
shukrani kwa kuleta hili