Hivi Kenya tatizo ni Nini?

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Kama kuna kiumbe anaweza kunielewesha nitashukuru, kwa maana nimekuwa sielewi kinachoendelea nchini Kenya, kulikuwa na uchaguzi wa Uraisi, wabunge ukaisha washindi wakapatikana, akiwemo Raisi mpya Bw.Uhuru Kenyata sasa ni kwa nini kila siku mara maandamano hapa, mara fujo pale mara hawa hawamtaki Raisi Uhuru, mara sijui wanataka kumtoa kwa maandamano, sasa hii yote ni ya nini?

Kama kulikuwa na Uchaguzi na Mshindi akapatikana kwa nini wote msiungane na kushirikiana naye mpaka Uchaguzi mwingine utakapofika? Tatizo ni nini? Na kama hawamkubali Mshindi ni kwa nini hata wanafanya Uchaguzi na kupoteza fedha nyingi za walipa kodi?
 
Mambo ya Wakenya waachie wenyewe..
Hata mjadili vipi hapa siasa za Kenya ni utata mtupu tangu wapate uhuru, ni kuuana tu na ukabila unawatafuna.
 

Wewe yakenya yana kuhusu nini?Tanzania kuna matatizo kibao ya wewe unataka kujua habari ya kenya kilaza wewe!
 
khaaaaaaa! mmempa mwenzenu za uso mpaka aibu, kha! :A S 109: :A S 109:
 
Wajanja wajanja sana sasa wamekuwa wengi na wamejuana yaani ni kama mpemba na mchaga wamelala chumba kimoja!!!!!!!

Unajua hiko kisa????!!!!
 
At least World cup is over....bunge la katiba MUPYA kurejea rasmi soooon...
 
Uchumi wa kenya ndo unadondoka hivyo alshabaab na mengineyo, ukabila utasitawi zaidi kuanzia sasa kikuyu na luya imeingia hadi kwenye terrorism sasa
 
Wewe yakenya yana kuhusu nini?Tanzania kuna matatizo kibao ya wewe unataka kujua habari ya kenya kilaza wewe!

Sijaona mantiki yyte ya kumjibu kwa lugha isiyo ya kistaarabu,ni bora kama mada imekukera ukapita kimya tu.
 
mambo ya wakenya waachie wenyewe..
Hata mjadili vipi hapa siasa za kenya ni utata mtupu tangu wapate uhuru, ni kuuana tu na ukabila unawatafuna.
yanatuhusu sana mtu asiye na akili ndio ataona hayatuhusu.wakidundana watakimbilia hapa kwetu na kuanza kugombania chakula kidogo tulichonacho.
 
Kijakazi hata kama CORD wangeshinda JUBILEE wangefanya kama CORD wanavyofanya. Usiombe UKAWA ya Tanzania ukawa kama ulivyo 2015 hakutakuwa na utofauti - sema Kenya kuna ile pronounced tribal/ukanda overtone
 
Kenya hakuna tatizo ni mambo ya demokrasia tu yanaendelea. Taifa linalokuwa na changamoto za ukinzani lina fursa kubwa zaidi kuendelea kuliko taifa lisilo na demokrasia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…