Hivi kumiliki gari ya safari ndefu Kama Toyota Prado kwa safari fupi za mjini ni akili au ujinga?

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Toyota Prado ni gari mahususi ambayo imetengenezwa kwa ajili ya safari ndefu Sio mizinguko mifupi fupi ya mjini.Hivi mtu kumiliki Hilo dude kwa safari za mizunguko ya mjini Ni akili au ujinga?

Sio matumizi mabaya ya pesa ?
 
Kuna mtu hata ile kukuona wewe kuwa JF ni ujinga. Haya maisha tu, kila mtu anayapeleka anavyotaka yeye alimradi haingilii uhuru wa wengine na kuvunja sheria za nchi. Ujinga au akili ni jambo la mhusika.
 
Actually Prado is the town car. Sio za safari ndefu. Land cruiser vx ndio habari nyingine.
Hata hizo VX watu wanazo za kutembelea mjini Kutoka saluni Moja kwenda saluni ingine.Unaukuta mdude huo kajimama kanapaki kanashuka kanaingia saluni kusuka nywele za mtindo wa mwenda kilioni
 
Toyota Prado ni gari mahususi ambayo imetengenezwa kwa ajili ya safari ndefu Sio mizinguko mifupi fupi ya mjini.Hivi mtu kumiliki Hilo dude kwa safari za mizunguko ya mjini Ni akili au ujinga? Sio matumizi mabaya ya pesa ?

Hakuna gari ya masafa marefu na mafupi kwa sense hiyo. Ni Hali yako ya uchumi tu....Prado kwa mjini Kama waimudu ni gari nzuri sana...!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…