Hivi kuna faida yeyote ya kusoma mpaka PhD ikiwa una 'gentleman' GPA?

JAMBONIA LTD

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2014
Posts
584
Reaction score
274
Habari wa kuu, kama swali lilivo ningependa kujua kama mtu ana GPA za lower divisions , kisha anakazana kusoma Masters mpaka PhD, kuna opportunities gani atapata maana tumezoea hayo kwa academicians...
 
Tuanzie hapa kwenye Gentleman GPA ni za aina gani?
 
PhD is primarily for academicians mana kwao ni takwa la msingi. Sasa mtu ambaye si mwanataaluma akiishia masters inatosha.

Lakini pia sio mbaya labda analenga kufanya kazi kwenye mashirikia binafsi/umma ambayo huwatumia watu wenye PhD katika nafasi za uongozi bila ya kigezo cha GPA ya shahada ya kwanza.

Kama msingi wa kusoma kwake ni huu wa pili basi ni sawa ila kwenye taaluma hawezi kwenda kwa gentleman degree. Lakin pia elewa PhD inafungua fursa mbalimbali pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Gentleman GPA zinapatikana kwa namna gn?
 
Huwa wanaolazimisha kusoma mpaka uzamili nanuzamivu hutumia pesa nyingi kuandikiwa kazi za shule. Ukweli unabaki pale pale akili zinabaki kwa anae kuandikisha. Ukikutana na wenye uwelewa wanagundua uwezo wako wa kujieleza na kujibu maswali ni mdogo sana. Zile course work huwa zinakuandaa na kukujenga kwa maisha hayo.
 
Mtu unaweza kusema masters ni professional degree na Ph.D. ni research degree. Kama wewe unafanya kazi kwenye shirika kubwa hasa yale ya uzalishaji na uko kwenye kitengo cha "research and development" Ph>D. kwako ni lazima. Kwa hiyo jibu la swali hili ni "inategemea na kazi yako. Kuna sehemu nyingine hata kama si academician, Ph.D. ni lazima.
 
 
Doh vijana wa siku hizi hawatumii hii terminology ya Gentle man GPA kumbe, maana naona imekua ngeni hali ilikua ni normal terminology by that time sorry..ni zile GPA za lower division.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…