Hivi kuna kipimo kinachoweza kuonyesha kama mtu alivuta bangi au alitumia madawa ya kulevya?

Naomba kujua kama kuna kipimo cha kitaalamu kinachoweza kuonyesha kuwa mtu fulani katika kipindi fulani cha maisha yake aliwahi kutumia bangi au aina nyingine ya madawa ya kulevya.
Kipo ni city scan, tulimpeleka mtu mzima pale muhimbili alipata strock, baada ya majibu Dr alisema huyu amewahi kuvuta sigara, na katika maisha yetu hatujawahi kumuona akivuta, tulipouliza wakubwa walikubali, kuwa mara ya mwisho kuvuta sigara ilikuwa mwaka 1964
 
Kipo kinaitwa Drug Urine Test(DUT) kina pima Cannabis(bangi) Ila kwa mtu alietumia Mara ya mwisho wiki 4 mpaka 5 zilizopita, heroin na opiods nyingine, methadone, diazepam, cocaine, tetra cyclic antidepressants(TCA), methamphetamines
Drug Urine Test
 
So far this is the best answer kwasababu nilitaka kujua hasa wale waliotumia vilevi hivi miaka mingi iliyopita.
 
Vipi hali yake kwa sasa , ameweza kuchechemea kidogo ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…