Kubaka kunafanyika pale ambapo uke unaingiliwa bila idhini ya mwenyenao. Hakuna tafsiri nyingine zaidi ya hiyo.
Hata statutory rape hakuna? Jimama la miaka 45 likifanya mapenzi na kivulana cha miaka 13, kwa mujibu wa sheria za Tanzania ni poa tu?
Miaka 13 inakakamaa??
Mwanamme anabakwaje? Naye anapata michubuko?
Lakini kubaka si lazima mtu atumie maguvu.
Hata kulala na mtu ambaye hajielewi vizuri - say aliye under the influence ya pombe au madawa au ambaye ana hitilafu za kiakili au mlemavu, kwenye baadhi ya nchi hiyo inahesabika kama kubaka kisheria (statutory rape)
Sheria ni ile ile mkuu sema vigezo, ushahidi mkubwa ni Dr. athibitishe kuwa ni kweli umebakwa, na ili uwe umebakwa kuna michubuko sehemu za siri na pia ukutwe na mbegu za kike. mwanamke anauwezo wa kupata ushahidi huo wote je mkuu wewe utaonesha nini? angalia usije ukajikuta umejipeleka mwenyewe polisi, maana ktk kubakwa mwanamme anaweza akajikuta kashiriki kusaidia kubakwa 100% hadi mbakaji ngoma ikawa nzito kwake akajikuta kachubuka sasa mpeleke polisi wewe, yeye akaonyeshe michubuko utajikuta unachezea miaka 30 bure bora hata unyamze iwe siri yako. wanaume wengi wanabakwa mkuu ila kushitaki inakuwa ngumu kidogo. Halafu angalia mwanamke sio wa kumpeleka polisi kirahisi rahisi kwa kesi kama hiyo, hakawii kukugeuzia kibao.
wewe ni jinsia gani kwani? Maana naona unatumia neno kuingilia halafu unauliza kuhusu mwanamke kumwingilia mwanaume. Una maana gani labda unaposema mwanamke kumwingilia mwanaume? Yaani hili litafanyika kwa namna gani?