Kuna watu hawakuoa, lakini wameuguzwa vizuri tu kwa sababu wameishi vizuri na watu, au wana fedha za kulipia huduma nzuri, au wanajaliwa na ndugu zao.
Kuna wengine walioa, mke/ mume alipojua tu kwamba mwenzake anaumwa na talaka ikaanzia hapo hapo.
Kwa hiyo habari ya kuuguzana si ya msingi katika kuamua kuoa.
Hii inategemea n'tu na n'tu
Mi nikikaribia kuzeeka naoa ili nianikwe vizuri juani.
Hao watu ni wamatumbi?
Kwahiyo hapa unatuaminisha kwamba zamani wote walikuwa ni wacha mungu? mbona magereza yote na mahakama vilijengwa zamani hizo? sikubaliani na wewe hapa unaleta urongo.
Ikishategemea n'tu na n'tu tayari si lazima.
Wa Msanga tena, mpaka Kisiju na Namuhoro kote wapo.
Am too old for this.Unawaza pua na mdomo ww mmh
nimejaribu kukalia kichwa na bado sijaona umuhimu wa makalio.kama hujui umuhimu wa Makalio, jaribu kukalia kichwa...
hata yesu alisema kama unaweza kushinda zinaa bora usioe
Mkuu kwa Biblia ninayoifahamu mimi aliyesema maneno hayo ni mtume Paulo, maana hata yeye hakuwahi kuoa mwanamke, ndio alisema mkiweza muwe kama mimi, lakini maneno haya nasema mimi, na asemi bwana.Sio lazima, ndo maana wengine ni watawa na wanaishi. Hata mtume Paulo alisema mkiishi kama mimi bila kuoa ni vyema zaidi.
Wanajamvi,
Naomba mnijuze kwa wale wenye uzoefu na wale ambao bado hamjafanya maamuzi
Huna haja ya juoa, ile kitu kata uandae BBQ tuje kujichana
mara nyingi ULAZIMA wa kitu huja kutokana na dhana ya WAJIBU, na option huja kama hicho kitu ni HAKI... hivyo kwa maana zote ninazojua mimi (kisheria, kidini, kiserikali, kijamii nk) kuoa si lazima...ni hiari yako LAKINI isiwe sababu ya wewe kwenda kinyume na hali uliyoichagua...mfano kuwa na wapenzi wengi, kuwachezea watoto wa watu, kutembea na wake za watu, kuwaona waliooa ni wajinga..nk... (kwa tathmini inaonesha kuwa vijana wa siku hizi huchelewa kuoa, na wachache hufa bila ya kuoa kutokana na sababu mbalimbali katika changamoto za maisha bila ya wao wenyewe kuzijua na kuchukua hatua kuzifanyia kazi: mfano- uchumi, hali ya kifedha, majukumu ya kazi na masomo nk)