ninashndwa kuelewa unaogopa kuoa au kuoelewa kuwasababu umechuma mali peke yako hvyo ukija kuoa au kuolewa mkija kuachana mtagawana mali ambazo uliangaika mwenyewe kama ni hvyo bas usifikirie kuoa au kuolewa. Kuhusu jamii kumpendelea mwanamke sio marekan hata hapa tanzania ipo ila itafika kipind hata sisi wanaume tutakuja kudai uhuru wetu mana hii tabia ya haki sawa na mwanamke kipaombele hii itatumaliza
Of course unashindwa kuelewa, sijasema chochote kuhusu mie, nimeongelea tatizo la ndoa katika jamii moja.
Kimsingi, ndoa, ukiiondolea uturi wooote inayopakwa, ni taasisi ya kiuchumi. Proof ya hili angalia divorce rates katika jamii ambazo mchangia uchumi ni mmoja (baba - kama jamii za magharibi zilivyokuwa miaka ya mwanzo ya karne ya 20) na jamii ambazo baba na mama wote wana nafasi karibu sawa kiuchumi ( magharibi ya leo). Utaona jamii ambazo zina usawa wa kiuchumi talaka zinaongezeka.
Na hata huko nyumbani, hususan mijini ambako wake na waume wana nafasi zinazokabiliana zaidi kielimu na hivyo kiuchumi, talaka zinaongezeka. Mentality ya "utanibabaisha nini" inazidi.
Kwa hiyo ukikataa kwamba ndoa ina uwio wa kiuchumi utakuwa unakataa ukweli. Ndiyo maana machifu na waungwana wenye mali zao walikuwa wana wake wengi tangu hata kabla ya mkoloni. Maskini uoe wengi utawalisha nini?
Ukifanya ndoa itishie uchumi, kama nilivyotaja hapo juu kuhusu talaka za kinyamwezi, utakuwa unatishia ndoa moja kwa moja.
Unaweza kuuliza kwa nini nanukuu sana unyamwezini? Huko ndiko tunakoelekea maana washaanza kutupangia human rights na gay rights kesho keshokutwa unaambiwa kama nchi yenu haina child support inayomkata mshahara deadbeat dad hampati msaada.
Na sie uchumi wetu tegemezi, tutafanya nini?
Kwa hiyo penda usipende, ndoa ina dynamics za kiuchumi, hata kama ni kwa sababu tu kuoa ni status symbol katika jamii yetu na aliyeoa anaweza kupata ubunge kirahisi kuliko asiyeoa, ndiyo maana unaona kina January Makamba wanaoa halafu ndio wanaenda kugombea ubunge, strategy. Not to say there was no love.
Mie sioi sio kwa sababu ya uchumi, sina kitu na most likely nikitaka kuoa nitapata heiress au malkia wangu atakayeniongezea ari ya kufanya vizuri.
Mi sitaki kuoa kwa sababu niko too independent na kuoa kuta limit independency yangu. Sitaki kuripoti kwa mtu wala mtu kuripoti kwangu.