Hivi kwa nini siku hizi nyumba nyingi kina mama ndio wenye sauti kuzidi kina baba?

Sawa Dada yangu nakubaliana na wewe yote uliosema, sisi wengine JF ni Furaha tupu..kama thread yangu imekukwaza nisamehe dada yangu sirudii tena

Hata mimi najua JF ni furaha tupu ndio maana nilijimwaga kwa mawazo yangu, kumbe nikakukwaza, am sore....
 
Hapana sio kuongozwa na kina mama; tena mwenyewe umesema vitu vidogo vidogo; ni kweli dialy run na vitu vidogo vidogo ndani ya nyumba ni jukumu la mama; huwezi kuja kwangu kuazima pasi nikupatie ...............utamsubiri wife ama ?

Jamaa anataka mpaka ufagio wa chelewa au mboga atoe kibali mwanaume ?
 
mwanamke ni sawa na katibu mkuu na ndo mweka hazina, nyumba zote ambazo mama anamadaraka ndo zina maendeleo. ni kweli kuwa baba ni kichwa cha nyumba lakini mama ndo shingo na kama shingo sio imara kichwa hakiwezi kuzunguka wala kufanya kazi sawasawa.
 
Kuna jamaa yangu mmoja wife wake kampiga marufuku kutembea hovyo baada ya kazi..

Ukipita nyumbani kwake jioni jamaa kakaa nje na watoto wife hayupo..

eeh hyo kali na mshkaji katulia tuliiii ilo limbwataaaa au kupenda kwa kupitiliza hao ndo huwa wanapika na kufua nepi za watoto mama anakuwa kwenye vikao vya arus na saloon,balaa si kidogo
 

even GOD knew from very begining kuw wanaume peke yao hawawezi, akaona si vema wakae peke yao, hawa wanaume wanahitaji msaidizi!! mfano rahisi ni kuwa hawa wanaume ni WAGONJWA na mke ni NURSE, ikumbukwe kuwa nurse ndio msaidizi wa karibu sana wa mgonjwa, madaktari wapo kwa ajili ya kutibu MAGONJWA lakini nurse yupo kwa ajili ya kutibu MGONJWA! Hizo 'sauti' zinazozungumziwa ni sehemu ya huduma za nurse kwa mgonjwa!
 
Hakuna makosa ambayo sisi wana ndoa, hasa wanawake kujifanya kuwa una sauti kuliko mumeo. Jambo la busara ni wote kwua pamoja, na sio sisi wanawake kufanya kila tuwezalo kumtawala mwanaume! I tell you, huyo mwanaume atakushangaza siku moja.
 
mwanamke ni sawa na katibu mkuu na ndo mweka hazina, nyumba zote ambazo mama anamadaraka ndo zina maendeleo. ni kweli kuwa baba ni kichwa cha nyumba lakini mama ndo shingo na kama shingo sio imara kichwa hakiwezi kuzunguka wala kufanya kazi sawasawa.

Kuna vichwa vingine havihitaji shingo...........mathalani kichwa cha treni.....bila hicho hakuna safari lakini hakina hiyo shingo....na vipo vichwa vingine vingi tu havina shingo.....sintovitaja kwa misingi ya kimaadili hapa
 
Kuna vichwa vingine havihitaji shingo...........mathalani kichwa cha treni.....bila hicho hakuna safari lakini hakina hiyo shingo....na vipo vichwa vingine vingi tu havina shingo.....sintovitaja kwa misingi ya kimaadili hapa

Duuh zamani nillikuwa nakijua kichwa hiki kichwa kinachokaa juu ya shingo tena kichwa shurti kiwe juu ya vitu vingine, lakini kadri nilivyozidi kuwa mkubwa nikagundua kumbe kuna vichwa vingi tena vingine vinaning'inia kwa chini.... loh... ukubwa raha....!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…