Hivi kwanin kamisheni ya voda mwanzo wa mwezi inapanda sana hata kama una miamala michache halafu kadiri siku zinavyoenda hupungua kwa miamala ileile?

huko kwenu vipi

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2015
Posts
1,520
Reaction score
1,462
Habarini wanajamvi...

Hivi kwanini kamisheni ya voda inapanda sana mwanzo wa mwezi unapofika katikati speed hupungua?

Wakati miamala ni ile ile?
Nimejiuliza sana hili swali lakin sipati jibu pengine humu ndani mnaweza kunisaidia...

Kuanzia tarehe 1 hadi kwenye trh 15 hiv kamisheni inaongezeka kwa speed kubwa yaaan baada ya hapo kamisheni hu-stuck wakati miamala ni ileile kama ya mwanzo,yaan inaongezeka kwa kiasi kidogo sanaaaaaa....
 
Bila Shaka wewe sio mfatiliaji wamiamala yako kwaukaribu zaidi, unachokifanyia kazi ndio hicho unacholipwa. Labda uongelee swali lawateja wako kuwa kuanzia tarehe hizo upungua ila sio vingine mkuu
 
Bila Shaka wewe sio mfatiliaji wamiamala yako kwaukaribu zaidi, unachokifanyia kazi ndio hicho unacholipwa. Labda uongelee swali lawateja wako kuwa kuanzia tarehe hizo upungua ila sio vingine mkuu


Wateja ni wale wale na huwa nakagua Mara kwa Mara we sema sifanyi mwenywe m nakuwa kwenye mishe zingine kuna mfanyakazi...
 
Kila muumala commission yake inaonekana,hivyo kama una wasiwasi uwe unaangalia commission kila baada
muamala unaofanya
 
Usianze kumsingizia mfanyakazi eti anakuibia,kmbuka salio la kamisheni huwezi ukalitoa kabla ya voda hawajakuingizia tarehe 1
 
Hivi kwa mzunguko wa kawaida

Tigo pesa, m pesa, airtel money unaweza chukua sh ngapi kamisheni

Mwenye uelewa tafadhali
 
Mwaka jana lifanya m-pesa aise hii kazi nikupoteza muda,ilikuwa kama tarehe 1/4. Hadi tarehe 30/4 nikaja kuangalia kamishen elf 40 ndio mshahara,Nilichoka kweli na hapo nina kama miamala 300+,nilifunga siku hiyohiyo nikasubiri tarehe moja wanipe changu nikaachanayo, ushauri usitegemee katika majukumu yako bali ifanye tu kama kivutio cha wateja dukani kwako
 
Hapa ndo huwa nachoka, unakuta mtu anaacha kazi ya kuajiriwa alafu anaenda kufungua mpesa akisubiri kijicomission kidogo mwisho wa mwezi, ni sawa na kucheza makida makida.
 
Hata kwangu ilikuwa ivo niliacha ajira yangu nikasem ngoja nijaribu na huku kumbe ndio hivyo kabisa
Hapa ndo huwa nachoka, unakuta mtu anaacha kazi ya kuajiriwa alafu anaenda kufungua mpesa akisubiri kijicomission kidogo mwisho wa mwezi, ni sawa na kucheza makida makida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…