Kuna interview moja ya Ndayiragije na Clouds fm alipokuwa ndo kakabidhiwa Starz, alisema kwamba alipokuwa anasoma kozi ya ukocha ili kupata leseni daraja A ya UEFA nchini Germany alikuwa na wenzie wa Burundi kama 10 hv ambao aligraduate nao, lakn pía akasema kile chuo ndani ya miaka 3 walishapita raia wa Burundi takribani 100
Na akaongezea pía kuwa wengi wao wametapakaa nchi mbalimbali duniani kutafuta fursa za ukocha kwakuwa wengi wao wana leseni cha ukocha daraja A ya UEFA
Hvyo kwa namna hiyo unaweza kuona ni namna gani jirani zetu wamepush na wanapush sn ktk angle hio ilhali nchini kwetu watu kama kina Matola, Nizar Khalfan, Zubeir Katwila wapo timu kubwa afu vijana lakn hawana hata angalau leseni ya ukocha daraja B ya CAF
Wachache kama kina Hemed Morocco, Dennis Kitambi, Master Charles Boniface Mkwasa nk ndio angalau wamejiimarisha ktk vyeti