Hivi kweli huyu Kanoute angeweza kumzidi Chikwende Uwezo?

Chikwende alitufunga kule kwao tukaona bora tumsajili! [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Ingetumia gharama......
Inakotoka hamtaki kujua, wanao toa hizo hela wakilalamika loss mnasema wanaongea sana.
Hao wachezaji unaowaona ndio mnaendana nao kiuchumi.
Waulize tu kama familia zao wanaziendesha vema na kupigiwa makofi na wake na watoto wao tu hilo lingetosha kujifunza
Mtu anataka wasajiliwe wachezaji 10 ila wote wawe wazuri 100% bila kujiuliza gharama za kuwanunua ni kubwa na kuwalipa ni gharama zaidi.

Mtu analaumu wakati hachangii hata sh 1 kusajili mchezaji na eti mwisho anaumia kuliko waliotoa pesa [emoji23][emoji23][emoji23]
Mimi huwa siwalaumu viongozi wa timu hizi najua zipo dhoofu kiuchumi zinaishi kwa kutegemea pesa zisizo rasmi zaidi ya mifuko ya wapenzi wao tu.Leo unataka umsajili mchezaji wa Al Ahly tena yule wa first eleven umlipe sh ngapi kwa kipato kipi maana yule jamaa wa Kaizer Chiefs tu tuliambiwa analipwa milion 150 kwa Mwezi sasa kwa nini tusikomae na akina Kagere ambao kwa mwaka ndo wanalipwa hiyo? Kila mtu anakula kulingana na urefu wa kamba yake huo ndiyo ukweli tujipongeze kwa tulipofika si haba
 
Watu tumekaa kilawama sana.....
Eti wasajiliwe wazuri, hao walionekana wazuri huko walikotoka.
Mshara wa milioni nne utampata mchezaji gani awe level tunazotaka, hawa tunaowaona ndio level zetu na hapo wanapotufikisha ( makundi na robo ndio level zetu pia).
Msitake watu watumie hela zao za mifukoni kuwapa furaha nyie, Na hamkuwahi kuwa na shukrani kwa wanachotoa.
 
Sahihi
 
Kanoute mpira anajua sema alichofanya game ya jana anakijua yeye na mwalimu wake maana aligeuka mtembezi (sio yeye tu karibia wachezaji wote )tu uwanjani.
 
Mimi nadhani hatuwezi kutoa hukumu kwamba Simba haijasajili vizuri. Hii ni kwa sababu kwa wachezaji wapya ni Kibu na Kanoute pekee ndio waliopata nafasi ya kutosha.

Unasemaje mtu kama Banda ni mbovu, ambaye kacheza gemu kama nne tu na anaingia dakika ya themanini huko. Siku ile kaanza akafunga, na bado na nusra atoe assist sema Ajibu akakosa goli la wazi. Siku ile ya Red arrows kwa mkapa kaingia dakika ya 80 huko na pia nusra alitoa assist Morrison akaleta ujinga. Mchezaji kama huyu unasemaje ni mbovu?

Duncan Nyoni huwa akiingia japo dakika za mwishoni ila huwa anaonyesha ana kitu, sema ndio vile hajapewa nafasi ya kutosha. Sakho majeruhi yanamsumbua unasemaje mbovu?

Bado sijaona sababu ya kusema hawa jamaa ni wabovu.
 
Banda naamini ni mzuri ila Kanoute amepata game chance sana.

Duncani Nyoni toka aje huyu kocha hata benchi simuoni
 
Binafsi mpaka Leo naumia Chikwende kuachwa ,alishaanza kuzoea ligi ,alishafunga magoli , naamini msimu huu angekua Bora zaidi
 
Sawa.....
Simba winga zao ni Morrison na Dilunga asa sijui anacheza wapi hapo bwana Tatenda?
Ukiona mgeni anawekwa benchi na mzawa huyo mgeni ni wa kuachwa.
Chikwende na uyo mbwa banda au shoga sakho bora uchezeshe Adam salamba
 
Naunga mkono hoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…