Hivi kweli suluhisho la miundombinu mibovu inayopelekea kukatika katika ovyo umeme ni kwenda kununua umeme nje ya nchi? Tuweni serious kidogo

Hivi kweli suluhisho la miundombinu mibovu inayopelekea kukatika katika ovyo umeme ni kwenda kununua umeme nje ya nchi? Tuweni serious kidogo

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
Sote tunataka nchi yetu isonge mbele lakini tunachoka na kuumia mnoo tunapoona suala la umeme hapa Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 mfululizo likitumika kama kichaka cha upigaji wa watu fulani fulani na kuchezewa sarakasi za ajabu na wanasiasa.

Kwa muda mrefu sababu za kukosekana kwa umeme wa uhakika kwa muda wote ilikuwa ni uhaba wa uzalishaji wa umeme. Na sababu za kukosekana umeme wa gharama nafuu zikawa ni zile zile za kukosekana vyanzo vya maji vya kutosha kuzalisha umeme huo.

Ujenzi wa Bwawa la Nyerere ukaonekana ndio suluhisho kamili, bwawa likajengwa kwa gharama kubwa sana na kuweza kuzalisha umeme wa kutosha mahitaji yetu yote ya sasa, mahitaji yanayotegemewa siku za mbele na zaidi ya umeme wa kutosha kuuza nje.

Sarakasi zikaanza ghafla, kwanza tukaambiwa gharama za umeme hazitashuka na huenda zikaongezeka tofauti kabisa na kile tulichoaminishwa hapo mwanzo kuwa, mbali na uhakika wa kupata umeme basi tutapata unafuu mkubwa wa kuilipia hiyo nishati.

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Hatujakaa sawa, umeme ukaendelea kukatika ovyo ovyo mara kwa mara, sababu ikaelezwa ni kuwa ni kutokana na kuchakaa kwa miundo mbinu ya usambaji wa umeme ambayo inahitaji ukarabati mkubwa na endelevu hivyo tuwe wavumilivu maana baada ya muda miundo mbinu itatengemaa na hicho kilio kitasahaulika.

Sasa ghafla leo tumesikia mpango mpya wa serikali kutia saini mkataba mpya wa kununua umeme kutoka nje ya nchi (Ethiopia) ili kuweza kutatua changamoto za kukatika katika ovyo umeme hapa nchini hususani kwa mikoa ya Kaskazini. Hivyo changamoto ya kukatika katika ovyo umeme itakwisha kwa kununua umeme kutoka Ethiopia na sio tena kukarabati miundo mbinu chakavu ya usambazaji wa umeme hapa nchini!

Kuna namna hatuko serious!
 
Yaan maccm yaan maccm aisee naumia sn hapo unakuta huo mkataba kuna mapesa kibao ya watz watagawana maccm kiasi kingne ktakuwa knaenda kwny chama chao ndo maana katu hawawez kubali ondoka madarakan hawa hawawez labda kwa mtutu au jeshi liwaondoe au maandamano ya kumwaga damu za watz wasio na hatia
 
Sote tunataka nchi yetu isonge mbele lakini tunachoka na kuumia mnoo tunapoona suala la umeme hapa Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 mfululizo likitumika kama kichaka cha upigaji wa watu fulani fulani na kuchezewa sarakasi za ajabu na wanasiasa.

Kwa muda mrefu sababu za kukosekana kwa umeme wa uhakika kwa muda wote ilikuwa ni uhaba wa uzalishaji wa umeme. Na sababu za kukosekana umeme wa gharama nafuu zikawa ni zile zile za kukosekana vyanzo vya maji vya kutosha kuzalisha umeme huo.

Ujenzi wa Bwawa la Nyerere ukaonekana ndio suluhisho kamili, bwawa likajengwa kwa gharama kubwa sana na kuweza kuzalisha umeme wa kutosha mahitaji yetu yote ya sasa, mahitaji yanayotegemewa siku za mbele na zaidi ya umeme wa kutosha kuuza nje.

Sarakasi zikaanza ghafla, kwanza tukaambiwa gharama za umeme hazitashuka na huenda zikaongezeka tofauti kabisa na kile tulichoaminishwa hapo mwanzo kuwa, mbali na uhakika wa kupata umeme basi tutapata unafuu mkubwa wa kuilipia hiyo nishati.

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Hatujakaa sawa, umeme ukaendelea kukatika ovyo ovyo mara kwa mara, sababu ikaelezwa ni kuwa ni kutokana na kuchakaa kwa miundo mbinu ya usambaji wa umeme ambayo inahitaji ukarabati mkubwa na endelevu hivyo tuwe wavumilivu maana baada ya muda miundo mbinu itatengemaa na hicho kilio kitasahaulika.

Sasa ghafla leo tumesikia mpango mpya wa serikali kutia saini mkataba mpya wa kununua umeme kutoka nje ya nchi (Ethiopia) ili kuweza kutatua changamoto za kukatika katika ovyo umeme hapa nchini hususani kwa mikoa ya Kaskazini. Hivyo changamoto ya kukatika katika ovyo umeme itakwisha kwa kununua umeme kutoka Ethiopia na sio tena kukarabati miundo mbinu chakavu ya usambazaji wa umeme hapa nchini!

Kuna namna hatuko serious!
Kumbuka kuna umeme wa Gas hapo tulipewa mapambio yote kuwa bomba likifika Dar mgao utakuwa ni historia. Leo hii bomba liko Dar na uzalishaji wa umeme wa Gas ulianza muda mrefu. Kwanini tununue umeme toka Ethiopia? Au zinasakwa hela za kuhonga kwenye uchaguzi?
 
Kumbuka kuna umeme wa Gas hapo tulipewa mapambio yote kuwa bomba likifika Dar mgao utakuwa ni historia. Leo hii bomba liko Dar na uzalishaji wa umeme wa Gas ulianza muda mrefu. Kwanini tununue umeme toka Ethiopia? Au zinasakwa hela za kuhonga kwenye uchaguzi?
ccm ni matapeli
 
Qmmk shuaini kabisa ifike wakati hawa watu wasomewe hata Albadil this is too much.
 
Awamu hii hawana masihara kabisa na ulaji.
Wanahakikisha kinachobaki hazina ni kwaajili ya kulipa mishahara na posho tu.
 
Hisia za wananchi si zipo simba na yanga sasa ngoja muoneshwe kazi
 
Nchi ina mabwawa ya umeme na miradi ya Gas halafu bado tunaagiza umeme nje. Something smells fishy.
 
Hapo kuna upigaji mkubwa unafanyika. Hiyo kununua umeme naona ningeresha tu kutuzuga..
 
Sote tunataka nchi yetu isonge mbele lakini tunachoka na kuumia mnoo tunapoona suala la umeme hapa Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 mfululizo likitumika kama kichaka cha upigaji wa watu fulani fulani na kuchezewa sarakasi za ajabu na wanasiasa.

Kwa muda mrefu sababu za kukosekana kwa umeme wa uhakika kwa muda wote ilikuwa ni uhaba wa uzalishaji wa umeme. Na sababu za kukosekana umeme wa gharama nafuu zikawa ni zile zile za kukosekana vyanzo vya maji vya kutosha kuzalisha umeme huo.

Ujenzi wa Bwawa la Nyerere ukaonekana ndio suluhisho kamili, bwawa likajengwa kwa gharama kubwa sana na kuweza kuzalisha umeme wa kutosha mahitaji yetu yote ya sasa, mahitaji yanayotegemewa siku za mbele na zaidi ya umeme wa kutosha kuuza nje.

Sarakasi zikaanza ghafla, kwanza tukaambiwa gharama za umeme hazitashuka na huenda zikaongezeka tofauti kabisa na kile tulichoaminishwa hapo mwanzo kuwa, mbali na uhakika wa kupata umeme basi tutapata unafuu mkubwa wa kuilipia hiyo nishati.

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Hatujakaa sawa, umeme ukaendelea kukatika ovyo ovyo mara kwa mara, sababu ikaelezwa ni kuwa ni kutokana na kuchakaa kwa miundo mbinu ya usambaji wa umeme ambayo inahitaji ukarabati mkubwa na endelevu hivyo tuwe wavumilivu maana baada ya muda miundo mbinu itatengemaa na hicho kilio kitasahaulika.

Sasa ghafla leo tumesikia mpango mpya wa serikali kutia saini mkataba mpya wa kununua umeme kutoka nje ya nchi (Ethiopia) ili kuweza kutatua changamoto za kukatika katika ovyo umeme hapa nchini hususani kwa mikoa ya Kaskazini. Hivyo changamoto ya kukatika katika ovyo umeme itakwisha kwa kununua umnua umeme kutoka Ethiopia na sio tena kukarabati miundo mbinu chakavu ya usambazaji wa umeme hapa nchini!

Kuna namna hatuko serious!
Hiyo pesa ya kununua umeme nje itumike kukarabati miundombinu
 
Sote tunataka nchi yetu isonge mbele lakini tunachoka na kuumia mnoo tunapoona suala la umeme hapa Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 mfululizo likitumika kama kichaka cha upigaji wa watu fulani fulani na kuchezewa sarakasi za ajabu na wanasiasa.

Kwa muda mrefu sababu za kukosekana kwa umeme wa uhakika kwa muda wote ilikuwa ni uhaba wa uzalishaji wa umeme. Na sababu za kukosekana umeme wa gharama nafuu zikawa ni zile zile za kukosekana vyanzo vya maji vya kutosha kuzalisha umeme huo.

Ujenzi wa Bwawa la Nyerere ukaonekana ndio suluhisho kamili, bwawa likajengwa kwa gharama kubwa sana na kuweza kuzalisha umeme wa kutosha mahitaji yetu yote ya sasa, mahitaji yanayotegemewa siku za mbele na zaidi ya umeme wa kutosha kuuza nje.

Sarakasi zikaanza ghafla, kwanza tukaambiwa gharama za umeme hazitashuka na huenda zikaongezeka tofauti kabisa na kile tulichoaminishwa hapo mwanzo kuwa, mbali na uhakika wa kupata umeme basi tutapata unafuu mkubwa wa kuilipia hiyo nishati.

Soma Pia: Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Hatujakaa sawa, umeme ukaendelea kukatika ovyo ovyo mara kwa mara, sababu ikaelezwa ni kuwa ni kutokana na kuchakaa kwa miundo mbinu ya usambaji wa umeme ambayo inahitaji ukarabati mkubwa na endelevu hivyo tuwe wavumilivu maana baada ya muda miundo mbinu itatengemaa na hicho kilio kitasahaulika.

Sasa ghafla leo tumesikia mpango mpya wa serikali kutia saini mkataba mpya wa kununua umeme kutoka nje ya nchi (Ethiopia) ili kuweza kutatua changamoto za kukatika katika ovyo umeme hapa nchini hususani kwa mikoa ya Kaskazini. Hivyo changamoto ya kukatika katika ovyo umeme itakwisha kwa kununua umeme kutoka Ethiopia na sio tena kukarabati miundo mbinu chakavu ya usambazaji wa umeme hapa nchini!

Kuna namna hatuko serious!
Ndio tatizo la viongozi wasio na maono marefu na kudharau taaluma
 
Back
Top Bottom