Hivi mnalionaje Kundi letu la Chan 2020

Joined
Nov 21, 2018
Posts
29
Reaction score
26
Tanzania tumepangwa kundi D ambalo lina timu:- Tanzania, Zambia, Guinea na Namibia. jJe wadau wa mpira katika kundi hili hatuoni kwamba tutakuwa tumepata nafasi angalau kati ya mshindi wa kwanza au wa pili?

Binafsi mimi Naipenda sana Taifa stars na kocha weti Ndairagije na naamini ataweza kutuvusha.
 
timu ngumu hapo ni Zambia
Guinea ni ngumu kuliko Zambia, wanao nyota wakali wanaocheza ligi ya ndani wakiwemo wa Horoya na Hafia, Zambia vile vile wanao nyota wakali ligi ya nyumbani wakiwemo wanaocheza Zanaco na Nkana, Hata Namibia wako vizuri Wana timu nzuri ya wachezaji wa nyumbani. Tusipogangamala tutakuwa wa mwisho. Lakini yakifanyika maandalizi mazuri na kuchagua vizuri wachezaji walio katika form VPL tunaweza Pata nafasi ya pili.
 
Hata sisi tuna nyota wakali wanaocheza ndanda, singida utd na yanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…