Superb2014
JF-Expert Member
- Jul 29, 2017
- 9,266
- 7,426
inawezekana kipo kipindi nilipita nilianza biashara kwa mtaji wa shilingi 10,000/- baadaye mauzo yakawa mpaka 30,000 kwa siku huku nikitengeneza faida ya zaidi ya 15,000/- kwa muda mfupi tu.Aise kumbe ndiyo maana hatuwi matajiri;
Just imagine mtu ana elfu thelathini anaweza kuizalisha;
kweli akili ni nywele kila mtu ana zake.
Wow ilikua ni biashara gani mkuu! Unaweza kushare na sisi tujikwamue pia?👏inawezekana kipo kipindi nilipita nilianza biashara kwa mtaji wa shilingi 10,000/- baadaye mauzo yakawa mpaka 30,000 kwa siku huku nikitengeneza faida ya zaidi ya 15,000/- kwa muda mfupi tu.
tena kwa mtaji huo nilikuwa nafanya biashara ya jumla wao wanauza rejareja
Wow ilikua ni biashara gani mkuu! Unaweza kushare na sisi tujikwamue pia?[emoji122]
Ahsante! UbarikiweMtoto mzuri hivi unateseka!!
Kweli dunia haina huruma, uje nikupatie mtaji[emoji2221][emoji2221]
ha..aha..aha....we mzuri hivyo unaweza fanya?Wow ilikua ni biashara gani mkuu! Unaweza kushare na sisi tujikwamue pia?👏
Wow hongera ilikua biashara nzuri 50% si mchezo. Naweza kufanya vizuri tu mkuu usihofu huo uzuri ni hapo kwenye picha tu labda ila nipo kawaida sana 😒ha..aha..aha....we mzuri hivyo unaweza fanya?
nilikuwa nauza juice kwa jumla lita moja buku na wao wanachukua na kuuza kwa glass kwa wakati ule mia tano kwa siku nilikuwa nauza mpaka lita 30 kwa lita wao walikuwa wanatapa glass tatu za mill 350 kwa hiyo kwa lita walikuwa wanabaki na 500 iliwatosha. mimi nikipata karibu 50% kama faida
Mbona hakuna utani wowote ndugu?? Ameambiwa mahindi ya kuchoma. Mhindi mmoja unauzwa 200 -300 mbichi anauza 1000 hapo kuanzia mwenge kuja Mbezi bei ni moja. Akichoma mhindi mmoja anakata vipande 4 kwa 300ni 1200. Toa mtaji wa hindi moja 250=950 faida mara mahindi 30=faida tu 46,500 only to serious people akiuza mbichi mmoja buku to mtaji 250 faida ni 750×mahindi 30= faida ni 22,500. Tusiwadharau tusio wajua kwa mwezi 22,500×30=675,000 hana mkopo hafungwi masaa 14 kama teller. Kwamaana teller anakaa chamanzi au salasala anaamka saa11 awahi job na kutoka 11na nusu kufika wazo ni saa mbili jumla msaa 14 kwa mshahara wa laki5 huyu anawahi asubuhi ananunua mzigo anaendelea na mambo mengine kijiweni anaenda saa kumi kuanza kuuza mahindi. Bado tunaona utani
Mbona hakuna utani wowote ndugu?? Ameambiwa mahindi ya kuchoma. Mhindi mmoja unauzwa 200 -300 mbichi anauza 1000 hapo kuanzia mwenge kuja Mbezi bei ni moja. Akichoma mhindi mmoja anakata vipande 4 kwa 300ni 1200. Toa mtaji wa hindi moja 250=950 faida mara mahindi 30=faida tu 46,500 only to serious people akiuza mbichi mmoja buku to mtaji 250 faida ni 750×mahindi 30= faida ni 22,500. Tusiwadharau tusio wajua kwa mwezi 22,500×30=675,000 hana mkopo hafungwi masaa 14 kama teller. Kwamaana teller anakaa chamanzi au salasala anaamka saa11 awahi job na kutoka 11na nusu kufika wazo ni saa mbili jumla msaa 14 kwa mshahara wa laki5 huyu anawahi asubuhi ananunua mzigo anaendelea na mambo mengine kijiweni anaenda saa kumi kuanza kuuza mahindi. Bado tunaona utani
Duuh mkuu umequote uzi wa miaka 7 iliyopita? Huyo mtu bado tu atakuwa na hiyo hiyo 30K?Ushawahi wazia Kahawa. Mtaji wa mbuni ni 1600 ki pakti.
Jana nilibahatika kukaa kijiwe cha kahawa jirani na Mwanza food. Alikuja askari mtaafu ana utani uliokithiri ila niliambiwa amelewa. Kwa utani wake nilipenda sana ika bidi nimwongeze kilaji nikalipia 2000 nikamwambia akachukue alichopenda kunywa. Akaja na shymwa. Kwakua ni mpenzi wawatu na wanywaji wanajuana nikaona akachukua kikombe cha kahawa. Akajimiminia akampa na mwenzie akajimiminia sawa na yeye. Jamaa akachukua tena akanimiminia nae askari tena akaona kimebaki kimoja akalalama akasema sasa tunywe kwa vipimo akaisoma sikuwahi jua vipombe vya chupa ya plastiki huwa ni mils ngapi. Jana akatamka ni Mls 200.
Sasa nikajua kumbe vikombe vitano vya kahawa ni sawa na Mills 200
Hesabu ikaanzia hapo.
Kama vikombe vi5 ni mls 200 je lita moja ni mls ngapi??
Litamoja ni mls 1000 kwenyekichupa ni sawa na vichupa vitano ndio lita hivyo vikombe vitano(5×5=25) mara chupa tano ni Mls1000 sawa na lita moja kikombe kimoja 100×25 sawa na 2,500. Kile kipakt kimoja cha mbuni ni lita 5-6 hivyo sawa na kusema 2500×5=12,500 kwa mtaji wa mbuni na mkaa wa buku na maji lita 10 faida kamili ni 8000 kwa mtaji wa 4000 je kwasiku kijiwe kikiuza lita kumi nisawa na mtaji 5500 faida 16,000. Tuvidharauvyo ndivyo vilipavyo
Kwa mtaji wako huo nakushauri uFanye Biashara ya kununua na kuuza nguo za ndani za, na hasa zile za bei za kawaida za kike na kiume wakubwa na watoto kutoka Dar kariakoo.Wakuu naomba ushauri mi ni mfanya kazi katika shirika la ulinzi nataka kufanya biashara kama nina elfu thelasini nifanyie biashara gani?
Ndio ivo mkuu wapo wengine walianza na buku mbili , kuna ndugu yangu alianza na buku mbili tu alianza na pakti mbili za sigara , šema alianza kitambo sana zaidi Ya miaka kumi na ushehe , Sasa hivi yupo vizuri sana aisee ,ameshajenga na ana maduka matatu Hapa mjini, haya maisha hayana formula wallah , usidharau kidogo ulichonacho hicho hicho kinaweza kukutoaAise kumbe ndiyo maana hatuwi matajiri;
Just imagine mtu ana elfu thelathini anaweza kuizalisha;
kweli akili ni nywele kila mtu ana zake.
vp hii biashara bado iko vzuri? mana n muda unepita sasa!Mwambie mrs Tibaijuka angalau akukopeshe Tsh 1,500,000/=tu nenda kaagize marobota ya nguo ya special kutoka Uganda na mafurushi kama 2 ya viatu maana uganda ni wazalishaji wazuri viatu aina ya ( yeboyebo) na nguo kutoka Jinja textile mills ltd njia nzuri ni ya bukoba -mwanza kwa njia ya maji haina gharama ya ushuru mkubwa jamani hii biashara inalipa hakuna mchozo mimi imenitoa nilianza kidogokidogo. kwenye msimu huu wa sikukuu ya x mass natarajia kufungua LODGE HAPA JIJINI MWANZA si kutegemea nilipotokea na nilipo kwa sasa.Tanzania yeboyebo inavaliwa acha mchezo.
Habari, bado unafanya hii biashara hadi sasa?hongera sana kwa moyo wa uthubutu, labda nichangie jambo moja hapo! kuna gari inayoenda mikoani. huko gunia la mkaa hununuliwa kwa kati ya shilingi 5,000 mpaka 8,000. ukichanganya na ushuru gunia linafika kwenye around 15,000. gunia hilo huku huuzwa kati ya 25,000 mpaka 30,000.
nikuombe jambo moja. lipia gunia hilo kwa shilingi 15,000 (ikimaanisha gharama za kununua na ushuru) ukiliuza utapata faida ya shilingi 10,000 ama 15,000 kwa gunia. ikiwa na maana kuwa kwa mtaji wa 30,000 utapata magunia mawili ambayo yatakuletea 30,000 faida, Mungu akisaidia kila safari nitakuwa nakuletea magunia matatu ambayo kwako itakuwa shilingi 45,000 bado tena kama Mungumanaleta wepesi kuna uwezekano wa safari tatu mpaka nne kwa mwezi. kamw safari moja faida itakuwa 45,000 x 3 =135,000 kwa mwezi UTAKUWA UMETOKA.
mtaji wa 30,000 leo unaingiza 135,000
NB: 1. NITUMIE NAMBA YAKO KWENYE INBOX AMA HAPA HAPA
2. KAMA MKAA HUTAUZA UTANIRUDISHIA MWENYEWE (kwa matumizi ya nyumbani)
3. Nia ni kukwamuana ktk lindi la umaskini, shida, mateso na karaha
4. utalipia mkaa wako utakapofika kwako (dar)
MUNGU IBARIKI TANZANIA....MUNGU IBARIKI JF