Hivi mtu anatakiwa kulipa kodi mara ngapi?

Hivi mtu anatakiwa kulipa kodi mara ngapi?

Ziroseventytwo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
8,581
Reaction score
15,618
Sisi ni wafanya biashara ya mazao, tunanunua mazao kwa wakulima kule ulanga,tunalipa ushuru wa mazao wa tsh 2500/= kwa gunia hii ni kwa wilaya ya Ulanga. Tuikifika hapa ifakara, baada ya kukoboa tunalipa tena tsh 3000/= kwa gunia ushuru wa mazao hii ni kwa wilaya ya Kilombero. Ukifanya hesabu, gunia 100 utalipa tsh 250000/=(ulanga huko) ukikoboa gunia 100 unapata kgs 7200 au gunia 72*3000=216000+250000 za ulanga unapata 466000/= na siku za karibuni kuna watu/wahuni wapo pale kibaha mail 1 kwenye mzani, wanatusumbua eti wanataka leseni/kibali cha kusafirisha mazao! Swali, hivi hizi tunazolipa kodi/ushuru tunalipa mara ngapi? Inakuwaje bidhaa 1 ilipiwe kodi/ushuru mara 2? Kwani mpunga si ndio mchele? Tafadhali mtu anayejua elimu ya mlipa kodi anijuze?
 
Duh huu uzi una manufaa sana! Tafadhali mwenye kufahamu mambo ya kodi atueleweshe tafadhali, kwani hata ndugu yangu mwingine naye alikuwa analalamikia tatizo
 
Ushuru unalipwa mara Moja tu tena inatakiwa iwe asilimia 3 hadi 5 ya bei Dira kwa zao husika.jukumu la hivyo vizuizi Ni kukagua vithibitisho Kama umelipa ushuru ulikotokea,km wakigundua hujalipa ndio unatozwa.vizuizi havina jukumu la kukusanya ushuru Bali ukuguzi.
 
Na juzi kati nimesoma kwenye gazeti mojawapo la kila siku TRA nao washaanza kutia maguu kwamba unatakiwa uwe TIN ile ulipe kodi ya mapato
 
Back
Top Bottom