Hivi Mwezi Ujao Ranking Ya Vilabu Ya CAF, Si Biashara Anaweza Akawa Mbele YaYanga?

Ndio! ndio! ujue lengo hapa lilikuwa nini,Uto🐸 azidiwe tu na Biashara United ata ikiwezekana CAF wabadilishe utaratibu wa kufanya ranking🙄🙄
 
Je, umezingatia pia hizo 5 years, Yanga Hana point hata moja aliyoingiza?
Kwa hesabu ya msimu huu yanga wana point moja na Namungo ana point 2.5 ila kwa hesabu za msimu ujao kwavile yanga hawakufika makundi msimu huu, Yanga watakuwa wana point 0.5 pekee huku Namungo wakiwa na point 2 badala 2.5
Hivyo kwa vyovyote vile Biashara kama wataingia makundi watamzidi yanga kwa point. Ila wasipoingia makundi basi hawatomzidi Yanga point kwavile yanga watakuwa wana point 0.5
 
Msimu huu Yanga Wana pointi moja wameitoa wapi mkuu?
 
Msimu huu Yanga Wana pointi moja wameitoa wapi mkuu?
We jamaa unasoma kuelewa au unasoma kubishana? Maana nimeweka wazi kila kitu lakini bado kichwa chako kigumu kuelewa. Nimekwambia 5 year ranking inafanyika kila msimu mpya unapofikia. 5 year ranking kuelekea msimu wa 2021/2022 imechukua point ya misimu mitano nyuma ambayo
Ni msimu wa
1)2020/2021
2)2019/2020
3)2018/2019
4)2017/2018
5)2016/2017
Ndani ya hiyo misimu mitano Yanga walipata point 0.5 hivyo hizi point zinazidishwa na coefficient ya mwaka yaani
Msimu husika inakuwa na coefficient5
Msimu wa pili kutoka juu una coefficient 4
Wa tatu kutoka juu una coefficient 3
Msimu wa nne toka chini una coefficient 2
Msimu wa mwisho kabisa unakuwa coefficient 1
Hivyo kwa 5 year ranking ya msimu wa 2020/2021 Yanga wana point 0.5 zidisha kwa mbili inakuwa point 1 .

Baada ya timu kuingia hatua ya makundi katika msimu huu wa 2021/2022
CAF wanafanya tena 5 year ranking ambayo itatumika katika mashindano ya msimu mpya wa 2022/2023. Point zinachukuliwa kwa walioishia makundi mpaka kwa aliyechukua kombe msimu wa 2021/2022. Hapa CAF wanachukua tena matokeo ndani ya misimu mitano kwanzia msimu wa 2021/2022 mpaka msimu wa 2017/2018. Zile point 0.5 za yanga hazitozidishwa kwa coefficient 2 bali zitazidishwa kwa coefficient 1 na kuwa ni 0.5 .
 
Jana nilikuwa naona kwenye predictions za watu soka kutoka tovuti rasmi ya CAF wameonyesha Uto inaweza kurank namba 127 baada ya mechi za CAF zinazofuata😏😏
sisi tunaitafuta nafasi ya 48965 huko.

ranks hazina umuhimu kwetu.

Mission & Vision ya klabu sio kupanda ranks, bali ni kutwaa ndoo tu.
 
sisi tunaitafuta nafasi ya 48965 huko.

ranks hazina umuhimu kwetu.

Mission & Vision ya klabu sio kupanda ranks, bali ni kutwaa ndoo tu.
Kweli! kweli! hapo nimekupata mkuu, ndoo zenyewe si kama Mapinduzi Cup au zile za tupa taka hapa🙄🙄 au nimekosea jombaa🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…