Hivi naweza kubadilisha kozi chuoni?

king roja

Senior Member
Joined
May 4, 2012
Posts
141
Reaction score
7
Jamani naomba kuwauliza, me nimeomba kozi kupitia Tcu but ktk uwombaji nilijaziwa na kaka yangu, my fist kozi kiukweli sijapendezewa nayo. Je ikitokea nimechaguliwa kozi hiyo nina uwezo wa kuibadilisha na kusoma kozi nyengine ktk chuo husika ambacho nimechaguliwa? Naomba majibu ma great thinkers
 
unaweza kubadili kozi. utabadili wakati wa kufanya registration.
 
Kwa uzoefu nilionao, kama huna undugu na wakubwa fulani, inakuwa ngumu.
 
unaweza kubadili kozi. utabadili wakati wa kufanya registration.

ok asante mkuu, na je taarifa ya kubadili kozi kwa bodi ya mkopo utaipeleka mwenyewe au chuo husika?
 
Unaruhusiwa kubadili kozi ndani ya wiki mbili za mwanzo wakati wa registration! ila itategemea point zako kama zinakuruhusu kuingia kwenye kozi unayoitaka!
 
Jamani aksanteni sana! nimepata kitu hapa!!
 
Ok kuhusu point sijambo ninalohofia sana coz mm nina point sita za kujiunga na chuo. Nashukuru kusikia kwamba ninaweza kubadili kozi
 
kama umepata kusomea BA/SC EDUCATION inakua ngumu kubadilisha labda utoke kozi nyingne kwenda Education.But hiyo ni UDSM,sijajua vyuo vingne.
 
kama umepata kusomea BA/SC EDUCATION inakua ngumu kubadilisha labda utoke kozi nyingne kwenda Education.But hiyo ni UDSM,sijajua vyuo vingne.

kwa mfano umechaguliwa bachelor of education in special needs ukaibadilisha na kuchukua bachelor of education in policy, planning and management si inawezekana coz zote zimejiwekeza kwenye education?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…