African Believer
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 436
- 426
Natumai wana Jamvi wenzangu mu wazima wa afya tele. Kama ni wazima karibuni kwenye uzi wa malalamiko dhidi ya benki za Tanzania.
Kwa miaka mingi sasa nimekua mkopaji na mnufaika wa taasisi za kipesa hapa Tanzania hasa mabenki. Lakini cha kushangaza sijawahi patiwa elimu yoyote yenye manufaa kwa ajili ya mustakabali na ustawi wa biashara yangu.
Na badala yake mabenki niliyopitia yamekuwa yakiweka sheria zinazomkandamiza mteja, hasa pale biashara inapokua haiendi vizuri. Utawakuta wakilazimisha marejesho pasipo kutaka kumsikiliza mteja na kumpa ushauri ni nini cha kufanya ili aweze kuondokana na mkwamo unaomkabili.
Matokeo ya wakopaji kukosa malezi na elimu kutoka kwa mameneja pamoja na maafisa wengine wa benki wenye jukumu hilo, benki nyingi hapa nchini zimekosa ustawi kwani wateja wake wengi hujikuta wakishindwa kurejesha marejesho kulingana na muda uliowekwa hali inayopelekea kupoteza mali zao walizoweka kama (collaterals) dhamana.
Jambo hili limekua kikwazo cha muda mrefu na watu wanaogopa kukopa kutokana na kuona spidi ya watu kufilisiwa malizao na kupoteza makazi kwa kuuziwa nyumba zao walizoweka kama dhamana.
Najua kwenye jukwaa hili hawatakosa wawili watatu wakutueleza ni kwa nini hili limeendelea kuwa tabia ya mabenki yetu.
Karibuni wana Jamvi.
Kwa miaka mingi sasa nimekua mkopaji na mnufaika wa taasisi za kipesa hapa Tanzania hasa mabenki. Lakini cha kushangaza sijawahi patiwa elimu yoyote yenye manufaa kwa ajili ya mustakabali na ustawi wa biashara yangu.
Na badala yake mabenki niliyopitia yamekuwa yakiweka sheria zinazomkandamiza mteja, hasa pale biashara inapokua haiendi vizuri. Utawakuta wakilazimisha marejesho pasipo kutaka kumsikiliza mteja na kumpa ushauri ni nini cha kufanya ili aweze kuondokana na mkwamo unaomkabili.
Matokeo ya wakopaji kukosa malezi na elimu kutoka kwa mameneja pamoja na maafisa wengine wa benki wenye jukumu hilo, benki nyingi hapa nchini zimekosa ustawi kwani wateja wake wengi hujikuta wakishindwa kurejesha marejesho kulingana na muda uliowekwa hali inayopelekea kupoteza mali zao walizoweka kama (collaterals) dhamana.
Jambo hili limekua kikwazo cha muda mrefu na watu wanaogopa kukopa kutokana na kuona spidi ya watu kufilisiwa malizao na kupoteza makazi kwa kuuziwa nyumba zao walizoweka kama dhamana.
Najua kwenye jukwaa hili hawatakosa wawili watatu wakutueleza ni kwa nini hili limeendelea kuwa tabia ya mabenki yetu.
Karibuni wana Jamvi.