Hivi ni kweli kiwanja kupimwa ramani ya mipango miji ni gharama sana?

Hivi ni kweli kiwanja kupimwa ramani ya mipango miji ni gharama sana?

Makavenga

Member
Joined
Feb 16, 2019
Posts
16
Reaction score
20
Habari za saa hizi, wadau. Nimepata tatizo, nikasema nililete hapa JF kwa wadau ili nipate suluhu. Maana JF ni uwanja mpana, na kwangu mimi imeshanitatulia mambo mengi sana ambayo hata sikuomba ushauri.

Mimi nilinunua kiwanja. Kiwanja hicho hakikuwa na hati, lakini tayari kishapimwa. Process zote za kutengeneza hati nimezimaliza ila jambo moja tu ndilo limebakia: swala la ramani ya mipango miji.

Niliwaambia mbona pameshapimwa na copy ya ramani nilileta. Wakaniambia bado ramani ya mipango miji. Kilichonishangaza ni gharama zake. Nimeambiwa ni milioni 3 kupimiwa ramani ya mipango miji. Mwenyekiti anadai pameshapimwa tayari, lakini nikiwaambia wanasema ramani hiyo siyo ya mipango miji. Sijui kisheria ramani zinatakiwa ziwe ngapi. Hawataki kuniambia katika hiyo milioni 3, ya serikali ni ngapi.

Nahitaji msaada wa kujua gharama halali ya kupimiwa ramani ya mipango miji kwa kiwanja ambacho urefu na upana wake ni 20/40. Halafu ni kiwanja cha kujenga nyumba moja tu na eneo dogo la uwani, lakini bei ya kupimwa utasema nimenunua shamba. Nataka nijue gharama ya ukweli; sina shida kuwapa posho yao, hata iwe laki tatu.

Wizara ya Ardhi
 
Kama kiwanja kimepimwa tayari ramani ya mipango miji ipo, uliyokuwa nayo itakuwa ni surveyed plan. Eneo lipo sehemu gani, mkoa gani, wilaya gani?

Kama wamekwambia ramani ya mipango miji haipo ni wazi hilo eneo lote na wanaokuzunguka hawajapima na Kuna uwezekano mkubwa eneo ulilonunua limekatwa tu viwanja na lilitengenezewa sketch plan ambayo haijapitishwa bado.
 
Kama kiwanja kimepimwa tayari ramani ya mipango miji ipo, uliyokuwa nayo itakuwa ni surveyed plan. Eneo lipo sehemu gani, mkoa gani, wilaya gani?

Kama wamekwambia ramani ya mipango miji haipo ni wazi hilo eneo lote na wanaokuzunguka hawajapima na Kuna uwezekano mkubwa eneo ulilonunua limekatwa tu viwanja na lilitengenezewa sketch plan ambayo haijapitishwa bado.
Yeye ajenge tuu ukiwafuata snaa hao wa maofisini hakuna kitu utafanya,mbona sie huku Mikoani tunajenga na wanakuja kurasimisha? Wapo Watendaji wa Mitaa,wenyeviti walishakaimishwa kupanga maeneo
 
Kama kiwanja kimepimwa tayari ramani ya mipango miji ipo, uliyokuwa nayo itakuwa ni surveyed plan. Eneo lipo sehemu gani, mkoa gani, wilaya gani?

Kama wamekwambia ramani ya mipango miji haipo ni wazi hilo eneo lote na wanaokuzunguka hawajapima na Kuna uwezekano mkubwa eneo ulilonunua limekatwa tu viwanja na lilitengenezewa sketch plan ambayo haijapitishwa bado.
Picha ya ramani hii hapa
Katika hivyo viwanja changu Mimi kipo hapo
 

Attachments

  • IMG_20241123_062617.jpg
    IMG_20241123_062617.jpg
    775.6 KB · Views: 19
Picha ya ramani hii hapa
Katika hivyo viwanja changu Mimi kipo hapo
Kuliko uwape milioni tatu hao wapumbavu bora ujiongeze ishi vizuri na jamaa zako wa serikali ya mtaa upate kibali cha ujenzi uanze kujenga mwanangu. Hayo mambo mengine yatafuata yasikuumize kichwa nchi ngumu sana hii, wewe unapambana ufanye jambo lako wengine wanapambana kukuwekea kauzibe usitoboe.
 
Hapo wanakutafuta wakupige tu hawana jipya ila kama upo Dsm iyo issue hata Serikali ya mtaa huwa wanasolve vizuri tu

Kuliko uwape milioni tatu hao wapumbavu bora ujiongeze ishi vizuri na jamaa zako wa serikali ya mtaa upate kibali cha ujenzi uanze kujenga mwanangu. Hayo mambo mengine yatafuata yasikuumize kichwa nchi ngumu sana hii, wewe unapambana ufanye jambo lako wengine wanapambana kukuwekea kauzibe usitoboe.

Kuliko uwape milioni tatu hao wapumbavu bora ujiongeze ishi vizuri na jamaa zako wa serikali ya mtaa upate kibali cha ujenzi uanze kujenga mwanangu. Hayo mambo mengine yatafuata yasikuumize kichwa nchi ngumu sana hii, wewe unapambana ufanye jambo lako wengine wanapambana kukuwekea kauzibe usitoboe.
Nimeshagharamia kutengeza hati, siwezi kuacha.
Kuhusu kibali cha ujenzi tayari ninacho
 
Kwanza inaonekana hujui vizuri unataka nini:
Huwezi ukasema et umekamilisha zoezi zima la kutafuta hati, nyaraka, then ukambiwa huna TP plan.
Utaratibu wa mpaka unapata hati upo katika hatua zifuatazo:
1.Eneo liwe na Mchori wa Mipango miji. Hapa huwezi ukasema unaandaa kwa ajili yako peke yako, nop..lazima uchukue na majirani zako.Hakuna master plan ya kiwanja kimoja. Kuna TP ya eneo zima.Ndo maana wakakuambia hiyo gharama.
2.Pili kama TP tayari eneo litapaswa kuwa na mchoro wa upimaji - survey plan.Hapa ndo eneo linawekewa mipaka - mawe n.k
3.Umilikishwaji: Kwa kutumia taarifa za matumizi kutoka TP, ukubwa, mipaka, majirani, serikali za mitaa, taarifa zako binafsi, maombi yako mwenyewe kwa mkurugenzi wako, indemnity, affidavit na nyaraka nyingine utaenda kwa afisa Ardhi atakuanzishia miamala, utalipia then utaratibu utaendelea kwenda kwa commissioner, mpaka kwa msajili wa hati then utapata hati yako.
KUHUSU GHARAMA
Kwa mtu kukwambia unaweza kuona ni kitu chepesi..lkn ukiingia kuanza kucheza ndo utaelewa.
Kwanza kiukweli hakuna mtumishi wa uma atoke ofisini, kwa ajili yako aende serikali za mitaa, kwa ajili ya kusainisha nyaraka zako..wanachofanya watakupa list uende ukusanye mwenyewe..kitu ambacho kinasumbua, sio mchezo inakuaga nenda rudi - mwaka, miaka miwili sababu ya DOCUMENTATION.
Ndo maana ukienda kwa mtu atakuambia 3M...huo usumbufu, hao matown planner mfano tu hawasaini bure, mashine wengi hawamiliki ni expensive - ataenda kukodi -150,000 - 300,000/= kwa siku.
Na hapo akikosea data - akaambiwa arudi tena ambacho ni kitu cha kawaida..tena 150,000/= - 300,000/=
Na vigharama vya kijingakijinga kwa macho vidogo lkn ukijumlisha utakura 1.5M -bado kuna wanasheria n.k
USHAURI
1.Hao unaoongea nao nenda nao taratibu ili uhakikishe unaelewa vizuri.
2.Usiwe mbishi sana - jaribu kuwa polite hata kama kinafiki - ukiwa friendly wata-overlook baadhi ya vitu vidogo.Pia kazi za ardhi kwa sababu ya usensitivity wake kuna cross checking nyingi - watu wengi wanahusika hivyo ni rahisi sana kuchukua muda mrefu kidogo..Watu wakiona una elements za utata hata ukiwapa 3M wanaweza wasichukue.Inahitaji wateja waelewa sana.
3.Ili kuepusha gharama kuokoa gharama ya fedha nenda Halmashauri/Manispaa husika.waambie unachotaka wao watakupa majibu na mtaanzia huko huko.
 
Kwanza inaonekana hujui vizuri unataka nini:
Huwezi ukasema et umekamilisha zoezi zima la kutafuta hati, nyaraka, then ukambiwa huna TP plan.
Utaratibu wa mpaka unapata hati upo katika hatua zifuatazo:
1.Eneo liwe na Mchori wa Mipango miji. Hapa huwezi ukasema unaandaa kwa ajili yako peke yako, nop..lazima uchukue na majirani zako.Hakuna master plan ya kiwanja kimoja. Kuna TP ya eneo zima.Ndo maana wakakuambia hiyo gharama.
2.Pili kama TP tayari eneo litapaswa kuwa na mchoro wa upimaji - survey plan.Hapa ndo eneo linawekewa mipaka - mawe n.k
3.Umilikishwaji: Kwa kutumia taarifa za matumizi kutoka TP, ukubwa, mipaka, majirani, serikali za mitaa, taarifa zako binafsi, maombi yako mwenyewe kwa mkurugenzi wako, indemnity, affidavit na nyaraka nyingine utaenda kwa afisa Ardhi atakuanzishia miamala, utalipia then utaratibu utaendelea kwenda kwa commissioner, mpaka kwa msajili wa hati then utapata hati yako.
KUHUSU GHARAMA
Kwa mtu kukwambia unaweza kuona ni kitu chepesi..lkn ukiingia kuanza kucheza ndo utaelewa.
Kwanza kiukweli hakuna mtumishi wa uma atoke ofisini, kwa ajili yako aende serikali za mitaa, kwa ajili ya kusainisha nyaraka zako..wanachofanya watakupa list uende ukusanye mwenyewe..kitu ambacho kinasumbua, sio mchezo inakuaga nenda rudi - mwaka, miaka miwili sababu ya DOCUMENTATION.
Ndo maana ukienda kwa mtu atakuambia 3M...huo usumbufu, hao matown planner mfano tu hawasaini bure, mashine wengi hawamiliki ni expensive - ataenda kukodi -150,000 - 300,000/= kwa siku.
Na hapo akikosea data - akaambiwa arudi tena ambacho ni kitu cha kawaida..tena 150,000/= - 300,000/=
Na vigharama vya kijingakijinga kwa macho vidogo lkn ukijumlisha utakura 1.5M -bado kuna wanasheria n.k
USHAURI
1.Hao unaoongea nao nenda nao taratibu ili uhakikishe unaelewa vizuri.
2.Usiwe mbishi sana - jaribu kuwa polite hata kama kinafiki - ukiwa friendly wata-overlook baadhi ya vitu vidogo.Pia kazi za ardhi kwa sababu ya usensitivity wake kuna cross checking nyingi - watu wengi wanahusika hivyo ni rahisi sana kuchukua muda mrefu kidogo..Watu wakiona una elements za utata hata ukiwapa 3M wanaweza wasichukue.Inahitaji wateja waelewa sana.
3.Ili kuepusha gharama kuokoa gharama ya fedha nenda Halmashauri/Manispaa husika.waambie unachotaka wao watakupa majibu na mtaanzia huko huko.
Kufupisha mambo atafute vishoka tu wamfanyie hiyo shughuli, vingenevyo atazunguka na kusumbuka sana.
 
Hivi ni Kweli Kiwanja kupimwa ramani ya mipango miji ni gharama Sana

Habari za saa Hizi wadau
Nimepata tatizo,nikasema nililete hapa Jf kwa wadau ili nipate suluhu.
Maana JF ni uwanja mpana
Kwangu Mimi imeshanitatulia mambo mengi Sana ambayo hata sikuomba ushauri.

Mimi nilinunua kiwanja
Kiwanja hicho hakikuwa na hati.
Lakini kupimwa tayari Kiwanja kishapimwa.

Process zote za kutengeneza hati nimezimaliza ila jambo moja tu ndio limebakia
Swala la ramani ya mipango miji.

Niliwaambia mbona pameshapimwa na copy ya ramani nilileta.
Wakaniambia bado ramani ya mipango miji.

Kilichonishangaza ni gharama zake
Nimeambiwa ni million 3 kupimiwa ramani ya mipango miji.
Mwenyekiti anadai pameshapimwa tayari,nikiwaambia wanasema ramani hiyo sio ya mipango miji
Sijui kisheria ramani zinatakiwa ziwe ngapi.
Hawataki kuniambia Katika hiyo mill3 ya serkali ni ngapi.

Nahitaji msaada wa kujua gharama halali ya kupimiwa ramani ya mipango miji Kiwanja ambacho urefu na upana wake ni 20/40 ?
Halafu ni Kiwanja cha kujenga nyumba moja tu na eneo dogo la uwani lakini bei ya kupimwa utasema nimenunua shamba.
Nataka nijue gharama ya ukweli Sina shida kuwapa posho yao Hata iwe Laki tatu.
kiwanja wakati unanunua ...ulinunulia chini serikali ya mtaa au utaratibu ulikuwaje? hapa ndo kuna chanzo na solution ya tatizo lako
 
Back
Top Bottom