Hivi ni kweli kuna wanyama ukiwagonga hupati kesi?

Hivi ni kweli kuna wanyama ukiwagonga hupati kesi?

aise

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2018
Posts
5,175
Reaction score
16,488
Habari wakuu, kuna jambo nimelisikia mara kadhaa watu wakisema, kuwa kuna baadhi ya wanyama au ndege ukiwagonga wapo ambao unashitakiwa na wapo ambao hakuna kesi ila kibinadamu unamalizana tu na mmiliki.

Kwa mfano ukigonga bata au kondoo, hapo kesi ipo na itafika mbali.
Ila kama utamgonga mbuzi hapo hamna kesi, hauwezi kushtakiwa,
Hiyo ni kweli au ni stori za vijiweni?
 
Story tu hizo. Dar es salaam my City Kuna Sheria ya Jiji inakataza kufungulia mifugo nnje. So ukimgonga mnyama yyt barabarani mmiliki wa huyo mnyama ndie anae paswa kushtakiwa .
Aise
 
Pia sheria za Highways, pedestrians hawaruhusuwi ila sehemu maalum labda ya kuvukia,wanyama it's a NO,pikipiki zote zenye cc ndogo haziruhusiwi, but Tanzania tuende nayo hivyo hivyo
 
"Onyo /tahadhari: mbele kuna katisho la wanyama wafugwao"

Hilo onyo huwekwa maeneo yenye wafugaji na mara nyingi ni nje ya miji!!!

Ukigonga mnyama kwenye huo ukanda/eneo, utawajibishwa..
 
Pia sheria za Highways, pedestrians hawaruhusuwi ila sehemu maalum labda ya kuvukia,wanyama it's a NO,pikipiki zote zenye cc ndogo haziruhusiwi, but Tanzania tuende nayo hivyo hivyo
Mkuu nchi zetu bado hazijafikia ustaarabu huo! Kwenye baadhi ya miji, barabara imezongwa na nyumba pande zote..

Maeneo kama hayo hawaweki vivuko maana vitakuwa vingi hivyo wanakuwekea alama tu itaķayokutahadharisha kuwa eneo hilo waenda kwa miguu wanakatisha punguza mwendo ongeza umakini!!!!

Vivyo hivyo kwa waendesha baiskeli na matela ya kukokotwa na wanyama..
 
Back
Top Bottom