Hivi ni kweli ni lazima serikali tatu?

Hivi ni kweli ni lazima serikali tatu?

Vujole

Member
Joined
Apr 3, 2013
Posts
33
Reaction score
22
Katika rasimu iliyozinduliwa Juni 03,2013 ili wananchi tuijadili na kutoa maoni kwa njia ya Mabaraza ya Katiba; kuna suala la Muundo wa serikali tatu. Mosi; nimejuiliza kwa nini Tume ilipendekeza iwe ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na sio Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Tanzania? Pili:kwa nini Tume imeona serikali ya Mapinduzi ya Zanziba na Serikali ya Tanzania Bara (ya Tanganyika kimantiki) lazima ziwe na Rais? Tatu;Kwa nini suala la rasilimali halikuweka kinagaubaga?
 
Haina maana ni wakati wa kila mmoja arudi kwao tuwe na Tanganyika yetu na wengine kimpango wao...Period.
 
tume ni ya muungano, hivyo imeshughulika na muungano; raslimali si suala la muungano. Kuhusu serikali tatu hili naona ili muungano uwepo lazima wawepo kwanza hao wanaoungana, yaani Tanganyika na Zanzibar; hao ndio waunde muungano. Kwangu majina si muhimu sana, la muhimu ni hiyo set-up.
 
Kwa mujibu wa heading yako ni kwamba UMEULIZA JIBU, ila kwa maelezo yako nadhani hujaipitia vizuri. Nenda kaisome tena.
 
Back
Top Bottom