Hivi ni kweli Yanga tumeushindwa kabisa Uchawi wa Mvua?

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Huko Algeria kinachoendelea muda huu kinasikitisha,na kibaya zaidi huu uchawi wameshajua ndiyo udhaifu wenu.

Niwaulize mashabiki na wadau wa Young Africans,ni kweli uchawi wa mvua mmeushindwa?

Kwanini kila mvua inaponyesha kwenye mechi zenu mmekuwa mkinyong'onyea?,naambiwa huko Algeria mvua haijanyesha miezi sita iliyopita,ila baada ya nyie kutia maguu tu mvua imeanza kupiga kila mualgeria anasherehekea kwa Kifaransa wengine kwa kiarabu,je,hii ina maana gani?


Hebu muambieni mzee mpili na wazee wenzie wafanye namna ili huu uchawi wa mvua utafutiwe ufumbuzi,mimi ni mtani wenu lakini napenda kombe litue nchini ili tuandike historia,japokuwa nafahamu kabisa kejeli zenu na matusi yenu yatanikosesha usingizi lakini sitaki kombe libaki Algeria itakuwa ni matusi makubwa kwa mpira wetu.

Naichukia sana Yanga ila kwenye hili niko pamoja na nyie,natamani kombe lije Tanzania ila kwa mvua zinazoendelea kunyesha huko ni asilimia 0.0000000001% wazee wa utopolo wanaweza kulileta hili kombe nchini.

Hebu mkitoka huko mkiwa na medali zenu za shaba mkifika pale utopoloni mwambieni mzee mpili msimu ujao wajitahidi suala la mvua mlipatie ufumbuzi.



Nikiripoti kitokea hapa Marekani,Ni mimi ndugu yenu Kolo niliye tukuka katika ujenzi wa Taifa.

Nikiwa na mshika maiki mwenzangu Kiranga katika moja na mbili.
 
Hayo mambo ya kuamini imani hizo ni ya akina Mwakarobo, Yanga tumefika hapa sababu ya pira la kisayansi na kuijengea timu yetu uwezo wa kushindana ndani ya uwanja hata kama leo tusipo toboa basi mwakani. Haya mambo ya mvua,kuota moto katikati ya uwanja ,hayo ni ya watoto wadogo kama wakina Mwakarobo.
 
Nilikua nashangaa wanaoandika yanga ikishinda wapigwe bann ila yanga ni wajinga tu kuamini mvua inawapa ushindi waarabu kwani iwanja si ule ule na watu si wale wale 11 kila upande iweje mtafute visingizio nyie pigweni mrudishe mashoga na vilema wenu hapa bongo. Wana simba nao wanawasubiri waje wawacheke yaani hamna pa kuchomokea kikubwa jitahidini mshinde na sijui mtawezaje kama hapa nyumbani mlishindwa tena kwa goli mbili kipi kitakua kimebadilika?
 
Vile Mbumbumbu likiteseka namna hii kwa povu zito haswa la kufulia hadi matusi juu huwa nahisi raha sana mimi Mwananchi [emoji38]

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Tukifungwa ni kama tumeshinda tu na tukishinda ndio hivyo tumeshinda tu. Mafanikio makubwa kwetu kufika fainali niseme nini kwa hatua hii ambayo Yanga wamefikia? Nitasherehekea leo usiku hata tukifungwa. Hii naamini ndio timu yangu bora kuwahi kuiona katika miaka yangu ya kuishi. Mpo na majungu tu wakati katika uhai wenu hamjawahi kushuhudia timu yenu ikicheza fainali katika mashindano ya Africa.
 
Uwanja uko hivi. Mimi nasema wakandwe tu hakuna jinsi nyingine
 
Wapigwe hadi wanye. Laana ya mgunda

Sent from my CPH2059 using JamiiForums mobile app
 
Yaani wewe hapo Mapipa ndio Marekani, yaani watu hadi akili zimechizi.
 
Kwenye mechi ya Yanga dhidi ya Us Monastir ya Tunisia uwanja wa Benjamin Mkapa, mvua kubwa tu ilinyesha! Na Yanga alishinda kwa 2-0!

Una maoni gani na hapa? Tena uwanja ulikuwa una mabwawa kabisa.

Na kuna mechi nyingine siikumbuki ilikuwa ni kati ya Yanga nani! Kwenye uwanja huo huo, bado walishinda. Ninachokumbuka mchezaji Bernard Morrison aling'ara sana kwenye hiyo mechi.
 
Wachawi wote hawapendi mvua maana ina haribu dawa zao.Mchawi haruki mvua ikinyesha maana dawa zinaweza kulowa akabaki hana kitu akakamatwa
 
Mnatukana mtu tena wa kwamsisi eti yeye ni ANDAZI halafu awaache salama? Kwa taarifa yenu Mvua itaendelea kunyesha mpaka mechi iishe
 
 
Kwani mkuu,kuna viwanja vingapi vitatumika leo kwa ajili ya hiyo match?
 
Mnatukana mtu tena wa kwamsisi eti yeye ni ANDAZI halafu awaache salama? Kwa taarifa yenu Mvua itaendelea kunyesha mpaka mechi iishe



Sipati picha itakavyokuwa kwa yanga na nyota yao ya moto! [emoji848][emoji4]
 
[emoji196][emoji196][emoji196][emoji196][emoji196][emoji196][emoji196][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…