Hivi ni nani Africa anayeweza kumfikia Abdulrahman Babu?

Hivi ni nani Africa anayeweza kumfikia Abdulrahman Babu?

Grand Master Dulla

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2012
Posts
411
Reaction score
148
Kusema kweli watu wengi wanaweza wasimjue lakini huyu mtu alikuwepo na bado yupo na ataendelea kuwepo. Si mwingine ninayemzungumzia hapo zaidi ya Abdulrahman Babu, kipenzi cha watu mwanamapinduzi wa kweli, shujaa na mtu mwenye akili nyingi sana na maono ambaye sijawahi kupata kuona mfano wake na mbadala wake.

Babu ni msomi aliyebobea na mwanauchumi mzalendo kwa bara lake. Sitaki kuongea mengi ila kila nikikaa nikifikiri bado nadhani nchii hii inahitaji kumfanyia kitu huyu msomi. Kumbuka reli ya TAZARA, kumbuka urafiki wetu na China na mengineyo mengi aliyoyaanzisha.

Kwa kifupi ni kwamba ili sisi tuweze kuendelea na kubarikiwa ni lazima tuonyeshe shukrani kwa watu kama hawa na wengine la sivyo mafanikio tutayasikia kwenye redio tu.

Nawasilisha...
 
inavyoonekana kizazi hiki kimekwisha,yaani hakun hata mtu mmoja anayejishughulisha na kujisomea wote wanahangaika na matumbo yao na kuganga njaa tu,mtu kienda kusoma anakimbilia masomo ya biashara kuzani kuwa ndio atafanikiwa au ndo fashion! jiulize unasoma hayo je we umfanyabiashara? je kutakuwa na wafanyabiashara wangapi? kama umesoma ili uajiliwe je wataajiriwa wangapi?
 
Kuna uzi nilisoma himu jamvini kwenye mwaka 2011kama sikosei. Ngoja niutafute niweke link hapa.
 
Babu alikuwa na akili nyingi sana sijawhi kupata kuona mfano wake,ila jambo la kushangaza sisi wenyewe hatumsamini,hivi unajua kwamba mandela na makomred wa ANC walimthamini sana babu na makomred wenzake kushinda hata mwlm mana walikuwa hawamwelewi baadhi ya mambo yake fulani fulani na baadhi ya maamuzi yake mana kulikuwa na shutma kali kutoka kwa baadhi ya wapigania uhuru wenye msimamo mkali waliokuwa nchini kuwa walikuwa na shaka naye.
 
Africa ukizaliwa na ukawa na akili nyingi kuliko watawala ni kosa.

Angalia yaliyomkuta Babu kwa Tanzania, Joshua Nkomo nchini Zimbabwe, Tom Mboya hapo Kenya, Kambona dhidi ya Nyerere nk
Hapo kwa Kambona naomba maelezo.

Nahisi umempa sifa ambazo hakuwa nazo.

Babu naunga mkono alikuwa kichwa sana lakini madai ya kumshinda mtawala napata shaka kidogo.

Ukweli ni kuwa wazee wengi wa zamani walikuwa vichwa hasa. Mfano hao akina Nyerere, Babu, ...., Dr. Aggrey, ....., n.k.
 
Haya ngoja tuitafute hiyo historian ya Babu, mana umechombeza tu habari kamili haipo
 
Haya ngoja tuitafute hiyo historian ya Babu, mana umechombeza tu habari kamili haipo

jitahidi kumjua vizuri huyu genius of our time na ukajifunza mengi sana kutoka kwake,jisomee mwenyewe usisubiri mbaka mzungu toka ulaya asome kwa ajili yako
 
alikuwa rafiki mkubwa sana wa walter rodney na walter alimkubali sana babu kiasi cha kumpa nfasi aandike katika kitabu chake maarufu cha how europe underdevelpd africa
 
Back
Top Bottom