jogoolashamba
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 348
- 71
WaTz janja ya nyani kwelikweli . Utaona watu wazima wa Bara wakilonga eti wana Serikali 2. Lakini ukiangalia kwa undani ni raia wa Zenj ndiyo wanatawaliwa na Serikali 2, yao na ya Muungano. Bara wana Serikali 1 ya Jamhuri ya Muungano. Utata huu wa watu wazima kuendelea kutumia maneno yenye kumaanisha hata jambo lisilokuwepo ndiyo asili yetu, migogoro haishi na kila wataalam wanapojaribu kuchanganua kiini cha mgogoro wanakufa ghafla. Professor Chachage na sasa Sengondo Mvungi.
Wazenj hawana noma kwani kwao wana chao kwanza ambacho hakiingiliwi na Bara. Bara je? Mwinyi alipokuwa Rais wa Tz aliwahi kutangaza wazi kuwa alikuwa amepewa kutawala Bara, Mzenj anatawala Bara. Masikini wote Bara hawakutaka hata kuuliza maana yake, walielewa lakini nani amvishe paka kengele? Mkubwa mmoja mpaka alifunikwa kanga kwenye sherehe ya hadhara, kama ishara ya kuwa mwandani wa wageni waliokuja kutawala nchi.
Hivi wote ni kasoro hatuelewi maana ya SERIKALI 2 TULIZONAZO, au huko juu hawana shida ya kujua maana kwa sababu wao malengo yao yanafanikiwa kimaisha?
Ili Bara wafanane na Zenj basi au sote tuwe na Serikali 1 ya jamhuri, au tatu kama wanavyosema wahenga, ya Bara isiyojuana na WaZenj, ya Zenj isiyojuana na Wabongo (ipo tayri) na ya Muungano ya wote Wabongo na WaZenj. Hivyo ndiyo Zenj watakuwa nazo 2 na Bara nao 2. Ni ujinga kujiita WABONGO huku tunaishi kama majuha ya kusukumwa na kwenda tu. Mimi mpaka natia mashaka Sengondo Mvungi wamemwondoa kwa sababu ya msimamo thabiti wa kutaka Serikali 3. Alikuwa msomi huyu na ushawishi wake ulikuwa maridhawa.
Mchezo wa "Ngamia kuingia ndani ya hema" ndiyo uliowashinda akina Njelu Kasaka na G8, la kushangaza WaZenj ndiyo wakapinga Bara kuwa na Serikali yao karibia wazipige kavu Bungeni.Bara anayekataa Serikali 3 basi anataka serikali 1, akitaka 2 nadhani akapimwe akili kwa "kuingiza ngamia ndani ya hema lake" mchana kweupe, au kalewa huyu hajui analolisema hivyo hafai kutusemea.
Wazenj hawana noma kwani kwao wana chao kwanza ambacho hakiingiliwi na Bara. Bara je? Mwinyi alipokuwa Rais wa Tz aliwahi kutangaza wazi kuwa alikuwa amepewa kutawala Bara, Mzenj anatawala Bara. Masikini wote Bara hawakutaka hata kuuliza maana yake, walielewa lakini nani amvishe paka kengele? Mkubwa mmoja mpaka alifunikwa kanga kwenye sherehe ya hadhara, kama ishara ya kuwa mwandani wa wageni waliokuja kutawala nchi.
Hivi wote ni kasoro hatuelewi maana ya SERIKALI 2 TULIZONAZO, au huko juu hawana shida ya kujua maana kwa sababu wao malengo yao yanafanikiwa kimaisha?
Ili Bara wafanane na Zenj basi au sote tuwe na Serikali 1 ya jamhuri, au tatu kama wanavyosema wahenga, ya Bara isiyojuana na WaZenj, ya Zenj isiyojuana na Wabongo (ipo tayri) na ya Muungano ya wote Wabongo na WaZenj. Hivyo ndiyo Zenj watakuwa nazo 2 na Bara nao 2. Ni ujinga kujiita WABONGO huku tunaishi kama majuha ya kusukumwa na kwenda tu. Mimi mpaka natia mashaka Sengondo Mvungi wamemwondoa kwa sababu ya msimamo thabiti wa kutaka Serikali 3. Alikuwa msomi huyu na ushawishi wake ulikuwa maridhawa.
Mchezo wa "Ngamia kuingia ndani ya hema" ndiyo uliowashinda akina Njelu Kasaka na G8, la kushangaza WaZenj ndiyo wakapinga Bara kuwa na Serikali yao karibia wazipige kavu Bungeni.Bara anayekataa Serikali 3 basi anataka serikali 1, akitaka 2 nadhani akapimwe akili kwa "kuingiza ngamia ndani ya hema lake" mchana kweupe, au kalewa huyu hajui analolisema hivyo hafai kutusemea.