Hivi sisi wala mihogo tunakwama wapi?

Hivi sisi wala mihogo tunakwama wapi?

Poker

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2016
Posts
5,445
Reaction score
14,828
Wakati wenzetu wakiendelea kuchanja mbuga huko kimataifa na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania, sisi wala mihogo kila siku ni visingizio na kutamba kumfunga Simba na unbeaten kwenye ligi ya mchongo.

Sisi mashabiki lia lia wa mihogo fc tumechoka hii hali tunataka nasisi tuwe na mafanikio kama ya simba huko kimataifa upande wa soka la wanaume na wanawake.

Leo hii Simba queens wametinga nusu fainali ila kwasababu sisi tunashindia mihogo kutwa kucha tunabeza hayo mafanikio yao, ila ukiuliza timu yetu ya yanga princess inafanya nini tutaishia kuitwa wala mihogo wameshiba na imewalevya.

Rai yangu kwa viongozi wa yanga haswa Eng. Hersi kuwa muungwana ujiuzulu nafasi yako aingie mtu ambaye atatupa mafanikio nasisi tufurahi kama Simba. Hongereni Simba queens nawatakia kila kheri mlete kombe nyumbani ili nasisi viongozi wetu waone wivu wamafanikio.
 
Wakati wenzetu wakiendelea kuchanja mbuga huko kimataifa na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania, sisi wala mihogo kila siku ni visingizio na kutamba kumfunga Simba na unbeaten kwenye ligi ya mchongo.

Sisi mashabiki lia lia wa mihogo fc tumechoka hii hali tunataka nasisi tuwe na mafanikio kama ya simba huko kimataifa upande wa soka la wanaume na wanawake.

Leo hii Simba queens wametinga nusu fainali ila kwasababu sisi tunashindia mihogo kutwa kucha tunabeza hayo mafanikio yao, ila ukiuliza timu yetu ya yanga princess inafanya nini tutaishia kuitwa wala mihogo wameshiba na imewalevya.

Rai yangu kwa viongozi wa yanga haswa Eng. Hersi kuwa muungwana ujiuzulu nafasi yako aingie mtu ambaye atatupa mafanikio nasisi tufurahi kama Simba. Hongereni Simba queens nawatakia kila kheri mlete kombe nyumbani ili nasisi viongozi wetu waone wivu wamafanikio.
🚮
 
Heirs sio shida shida ni wachezaji waposoft sana na hata wafundishweje wao nikufungwa tu
 
Labani og naona siku hizi amechoka kuitetea timu yake pendwa. Zile nyuzi zake za mapambio kwa wala mihogo fc hata sizioni
 
Mnakwama hapa!

1667776218183.png


Bahasha tatu: Mwamuzi wa kati ile bahasha nene zaidi. Wale washika vibendera zile bahasha mbili nyingine!! Mnajitekenya halafu mnacheka wenyewe kufurahia ushindi wa bahasha!! Maumivu ya kimataifa halali yenu!!
 
Back
Top Bottom