Hivi Traffic Police wa Kongowe Mwisho na SUMATRA, mnafahamu uhuni wa daladala za Kigamboni - Mwandege au mnakula 10%?

Hivi Traffic Police wa Kongowe Mwisho na SUMATRA, mnafahamu uhuni wa daladala za Kigamboni - Mwandege au mnakula 10%?

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2019
Posts
1,213
Reaction score
1,918
Nimekuwa mtumiaji wa hii route ya KIGAMBONI mpaka KONGOWE kwa muda mrefu nikiwa na safari kati ya Kigamboni na Mkuranga. Kwa ujio wa safari za daladala kati ya KIGAMBONI na MWANDEGE nilipata ahueni ya nauli na muda..

Na hii route madereva na makonda wengi walikuwa wakiipigia kelele wakijifanya kuwa itakuwa na usaidizi kwa abiria na wao wakipata hela maana nauli mpaka MWANDEGE ni kubwa.. Lakini cha ajabu toka hii route imeanzishwa kumekuwa na usumbufu kwa abiria kwa ukatishwaji wa safari zinapofika KONGOWE,na hii inafanyika bila kujali muda. Yaani iwe asubuhi, mchana, jioni au usiku route zinakatwa. Ila ni mbaya zaidi zinapofika muda wa usiku.

Sehemu maarufu zinazotumiwa na daladala kujificha ni Barabara kwenda SERIKALI YA MTAA KONGOWE na barabara ya MTAA WA KICHANGANI..
Sasa kama hizi daladala hazitaki hii route kwanini waliziomba? Halafu uhuni mwingine ni kuchukua nauli ya kwenda MWANDEGE wakati wanaishia KONGOWE..

Na Traffic Police wa KONGOWE-MWISHO wanayaona haya madaladala yakikatisha safari na hawachukui hatua yoyote, Na SUMATRA nao wako kukimbizana na vibali vya bodaboda badala ya hawa wahuni.
 
Nimekuwa mtumiaji wa hii route ya KIGAMBONI mpaka KONGOWE kwa muda mrefu nikiwa na safari kati ya Kigamboni na Mkuranga. Kwa ujio wa safari za daladala kati ya KIGAMBONI na MWANDEGE nilipata ahueni ya nauli na muda..

Na hii route madereva na makonda wengi walikuwa wakiipigia kelele wakijifanya kuwa itakuwa na usaidizi kwa abiria na wao wakipata hela maana nauli mpaka MWANDEGE ni kubwa.. Lakini cha ajabu toka hii route imeanzishwa kumekuwa na usumbufu kwa abiria kwa ukatishwaji wa safari zinapofika KONGOWE,na hii inafanyika bila kujali muda. Yaani iwe asubuhi, mchana, jioni au usiku route zinakatwa. Ila ni mbaya zaidi zinapofika muda wa usiku.

Sehemu maarufu zinazotumiwa na daladala kujificha ni Barabara kwenda SERIKALI YA MTAA KONGOWE na barabara ya MTAA WA KICHANGANI..
Sasa kama hizi daladala hazitaki hii route kwanini waliziomba? Halafu uhuni mwingine ni kuchukua nauli ya kwenda MWANDEGE wakati wanaishia KONGOWE..

Na Traffic Police wa KONGOWE-MWISHO wanayaona haya madaladala yakikatisha safari na hawachukui hatua yoyote, Na SUMATRA nao wako kukimbizana na vibali vya bodaboda badala ya hawa wahuni.
NDIOO UHAME MPWAA SHTUKAA KIDOGOO AMA
 
Trafiki ni moja ya viumbe wa ajabu kuwahi kuishi dunia baada ya zama za mawe.

Majuzi nilikuwa naenda kwenye mizunguko yangu nikawa naongea na konda wa daladala namna ambavyo hawa watu wasio na uchungu na mali za wenzao wanavyogeuza daladala kama ofisi zao.

Yule konda anasema kila siku analazimika kutoa 15000 hadi 20000 kwa hawa nyange nyange ili tu wasiwabambikie makosa. Yaani trafiki anasimamisha gari konda anasuka anampa 2000 akisogea mbele anafanya hivyohivyo. Wanasema usipowapa wanaanza kukagua gari wakikuta hata kosa dogo basi wanakuandikia faini.

Rushwa kwa trafiki ni kama imehalalishwa.
 
Fanya hivi kuwasaidia chukua tiketi yako nenda karipoti ofisini utaona mziki wake siku nyingine hawatarudia. Shida yetu huwa ni kulalamika tu bila kuchukua hatua.
 
Trafiki ni moja ya viumbe wa ajabu kuwahi kuishi dunia baada ya zama za mawe.

Majuzi nilikuwa naenda kwenye mizunguko yangu nikawa naongea na konda wa daladala namna ambavyo hawa watu wasio na uchungu na mali za wenzao wanavyogeuza daladala kama ofisi zao.

Yule konda anasema kila siku analazimika kutoa 15000 hadi 20000 kwa hawa nyange nyange ili tu wasiwabambikie makosa. Yaani trafiki anasimamisha gari konda anasuka anampa 2000 akisogea mbele anafanya hivyohivyo. Wanasema usipowapa wanaanza kukagua gari wakikuta hata kosa dogo basi wanakuandikia faini.

Rushwa kwa trafiki ni kama imehalalishwa.
Pengine hizi 2,000/= wanazotoa zinawapa ujeuri na kudharau taratibu za safari kwa kuwa dau lenyewe la Traffic Police dogo.
 
Back
Top Bottom