Hivi tulikosa mpambaji kwenye Mkutano wa nchi za EAC?

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Kusema kweli Wizara ya Mambo ya Nje mmeniangusha sana. Jinsi tunavyoandaa mikutano mikubwa kuanzia tunavyopamba maeneo yanapofanyika mikutano hiyo ni jambo la muhimu sana hasa katika kujenga taswira ya namna gani nchi hiyo ilivyo.

Kwa namna mapambo yalivyokuwa katika mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki napenda kusema tumejivua nguo. Tumepamba kana kwamba ni kikao cha Baraza la Madiwani la halmashauri ya Tanganyika. Hakuna maua, vitambaa vya hovyo, viti vya hadhi ya chini as if tulilazimishwa kwa kweli.

Nimesikitika sana. Safari hii Wizara ya Mambo ya Nje na Jumuiya ya Afrika Mashariki mmemiangusha sana.

Haya ndo maeneo ambayo kama nchi tunatakiwa tujiuze kwa uzuri wetu na namna tunavyoweza kufanya mambo kwa uzuri na ufasaha hadi kuvutia watu wengine waipende Tanzania.

Niishie hapa

 
january kaanza kuharibu na huku๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜๐Ÿ˜

Nitacheka sana kama hapa ni ngurudoto

Mapambo yakimasikini hata ngoma za kibao kata panapendeza kuzid hapa

Aibu
 
Mh, watanzania bwana; ukiwashinda kwa kila kitu basi wanaweza hata kukosoa kivuli chako kuwa ni cheusi sana.
 
CCM imezoea kupora kilakitu, ilitaka ijioneshe kuwa ndiyo iliyoandaa mkutano huo.
 
Ulitaka waweke maua na toilet papers ukutani?
 
Setting utadhani kijiwe cha Sangoma kwenye filamu za kinaijeria.

BTW:Kipara yupo hapo,ubabaishaje kama kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ