Hivi tuna sheria inayozuia kelele?

emalau

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2009
Posts
2,775
Reaction score
3,106
Wana janvi nimeleta mada hii baada ya kufikiri kwa miuda mrefu madhara yanayotokana na kelele lakini watanzania tunaonekana kutojali hata kidogo. Nimekuwa nilitembelea jiji la Dar es salaam nikapata shida sana, jirani ya hotel nilikokaa kulikuwa na mziki mkubwa, nilipouliza wenye hotel kuna nini jirani wakaniambia eti ni sherehe ya mtoto mchanga ya kufikisha siku arobaini !! Mziki ulipigwa usiku kucha nikaanza kujiuliza je huyu mtoto wa siku arobaini si wanamuua masikio? Sijafanya utafiti lakini ninahisi kuna watoto wengi watakaokuwa mazezeta kwa ujinga kama huu.

Nilipofika maeneo ya vijana nikakuta mziki unapigwa mango garden usiku kucha nikajiuliza watoto wanaoishi maeneo hayo wanafanya homework kweli? bila shaka watoto wanaoishi maeneo haya kitu homework hawakijui na uwezo wao wa kuperform shuleni lazima utakuwa wa chini tu.

Hapa jijini Arusha mji unakuwa kama hauna mwenyewe, unaweza kuwa uko ofisini asubuhi unaanza kazi ukasikia mziki mkubwa unapigwa na magari barabarani eti wanafanya matangazo, kwa kufanya hivyo wanafanya ufanisi wa kazi unashuka maana inabidi usubiri wapite ndo uendelee na kazi.

Kwa ujinga kama huu uchumi wa nchi unaweza ukawa unashuka bila kujua kumbe kuna sababu nyingine kama hizi ambazo viongozi wasioweza kufikiri kwa undani hawawezi kung'amua.

Naomba tujadili kama kuna sheria inayoweza kutusaidia ili tuwasaidie watoto wetu na sisi wenyewe, Kagame alishaagiza makanisa na misikiti kutoweka vipaza sauti maana mida ya ibada wanaifahamu.

Nawakilisha
 
Sheria ipo inaitwa "nuisense" inatumika kwenye kesi za madai chini ya criminal 'tresspass' kama kelele hizo zinaingilia uhuru wako wa "peaceful enjoyment' of your land!.

Ili uweze kufungua mashitaka shurti la kwanza ni wewe kama mshtaki lazima uwe unaishi eneo husika la karibu na hiyo disturbance ya sauti!.

Unaiomba mahakama
1. kuzuia hiyo kelele isiendelee kutolewa
2. Unaweza kudai fidia kama kelele hiyo imekusababishia madhara yoyote kimwili, (uziwi), kiakili (ukichaa) au kisaikolojia (disturbance ya peace of mind).
3. Pia unaweza kudai fidia kama kelele hizo zimekusababishia loss of income mfano mpangaji amehama au ni hoteli wageni wamehama au hupati wateja kutokana na kelele!.

NB. Kama ni kelele za adhana huwezi kufungua mashitaka!.

Pasco.
 
Sheria ipo inaitwa "nuisense" inatumika kwenye kesi za madai chini ya criminal 'tresspass' kama kelele hizo zinaingilia uhuru wako wa "peaceful enjoyment' of your land!.

Duh!

"nuisense" nayo ni sheria? Kaazi kweli kweli.
 
NB. Kama ni kelele za adhana huwezi kufungua mashitaka!.

Pasco.
Post yako ina makosa kadha wa kadha , ila naomba niweke msisitizo hapa kuwa nuisance au kelele km ulivyosema,haichagui adhana,mapambio wala nyimbo za kuambudu , adhana ikionekana inaleta usumbufu kwa mtu au watu wa aina yoyote,wana ruksa ya kwenda mahakamani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…