Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,112
Kile ulichotaka kutufahamisha ni kizuri,ila namna ulivyokiwasilisha ni tofauti.Tatizo ni kubwa wala siyo UDOM pekee hata vyuo vingine kuna wanafunzi wachache hawajalipwa tena hata wale wanaosoma nje ya nchi haswa China.Bodi ya mikopo imejaa mazuzu kiasi cha kutokuwa na Afisa ambaye anaweza kuwa mfuatiliaji wa malalamiko ya wanafunzi na kuyafanyia kazi.Wao ndoto zao ni kujaza magari kwenye viunga vya bodi wakisubiri wanachuo wagome ndipo wazinduke kutoa maelezo.Mwisho,nadhani umefananisha UDOM na High School kwasababu ya stress na shida za chuoni, Au kwa kuwa ni vigumu kutenganisha shule za kata,UDOM na ilani ya ccm. Serikali ya magamba isiwatese wanachuo kwani inajipalia mkaa,poleni UDOM!