Hivi udongo wanaokula wanawake wajawazito wa mjini unawasaidia nini? Na je, hauna madhara kiafya?

Hivi udongo wanaokula wanawake wajawazito wa mjini unawasaidia nini? Na je, hauna madhara kiafya?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Wakuu, mimi ni mkazi wa Tandika Mwembeyanga jijini DSM, mara kadhaa nimewaona wadada na wamama wa huku Tandika wale ambao ni wajawazito wakihaha kutafuta udongo ambao huutumia kama chakula, ningependa kufahamu faida wanazozipata kwa kula udongo huo ambao huuzwa kwenye magenge kadhaa kwenye eneo letu.

Kwa kadiri ya ufahamu wangu, udongo zaidi ya kuleta uchafu labda na minyoo kwenye mwili wa mtu sioni kingine ambacho mtumiaji anaweza kukipata, sasa labda kama kuna anayefahamu basi anijulishe faida wapatazo wanawake waja wazito wanaoutumia udongo kama chakula.
 
unatengenezwa na kiwanda gani mkuu?
Ni madini hayo natural yako ardhini. Kwa kawaida tunayapata madini hayo kwa kula matunda. Matunda yana absorb madini kutoka ardhini.

Kwa mahitaji ya ziada mama mjamzito anakuwa na cravings kwa udongo.
 
Si mzuri kiafya na ni hatari kwa mama na mtoto. Kuna kitu tunaita pica hii ni tabia ya mtu kula vitu vya ajabu kama plastic, vyuma etc. Inaonekana hii tabia hutokea baada ya mwili kusense upungufu wa madini fulani mwilini. Mama wajawazito huwa na uhitaji mkubwa wa madini chuma nk, inasemekana ndiyo hupelekea kupenda udongo. Ila kiafya siyo poa bora apige vidonge vya vitamins au apige misosi yenye vitamin za kutosha kama mayai, nyama, mbogamboga na matunda.
 
Ni madini hayo natural yako ardhini. Kwa kawaida tunayapata madini hayo kwa kula matunda. Matunda yana absorb madini kutoka ardhini.

Kwa mahitaji ya ziada mama mjamzito anakuwa na cravings kwa udongo.
Ikiwa ni hivyo kwanini wanaokula ni wanawake wa kiswahili tu, na mbona wizara ya afya imesahau kuwahamasisha wanawake wengine?
 
ikiwa ni hivyo kwanini wanaokula ni wanawake wa kiswahili tu , na mbona wizara ya afya imesahau kuwahamasisha wanawake wengine ?
Hamu ya kula inaletwa na cravings kama huna huwezi kutamani. Wengine Hypatia madini haya kwa kula matunda. Wizaracya afya inahimiza unajua wa matunda kwa wajawazito
 
Back
Top Bottom