Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Naunga mkono kauli hii asilimia 100% maana upuuzi huu umetamalaki sana hasa timu hizi mbili za Simba SC na Yanga FC, na kwanini viongozi wanakuwa wazito kushughulikia suala hili la utovu wa nidhamu au kuna namna fulani kati ya kiongozi au mchezaji?
Kwa kweli tabia ya mchezaji kupata jeraha la enka kidogo safari kwao naiona hapa nchini tu. Hivi wachezaji wa timu za ulaya wakiwa majeruhi wanaruhusiwa kirahisi kweli kwenda kwao kutatua matatizo yao ya kifamilia? Cha ajabu hata akipona bado harudi kwa wakati.
Na kama kocha anaponda utaratibu huu, je sisi mashabiki na wanachama tusemeje? Ni vema kuponda huu ujinga wa ruhusa kwa wachezaji wa kigeni kurudi kwao kwa matatizo ambayo hakuna ulazima wa kufanya hivyo.
Ligi ya VPL na Michuano ya Mapinduzi na FA ni michache sana kwa mchezaji kuitumikia klabu ambayo inamlipa fedha nyingi sana, lakini cha kushangaza Simba SC na Yanga FC ndo wako mbele kubariki utaratibu huu wa ruhusa kwa wachezaji mpaka wengine kuamua kulima na kupalilia shamba huko kwao Zambia.
Ni wakati sasa wakung'amu hili ambalo limeota mizizi, ninyi viongozi wa Simba SC na Yanga FC kuweka adhabu kali sana kukomesha ujinga huu wa mchezaji kula mshahara wa bure huku yuko kwao halafu timu ikivurunda kocha ndo mchawi.