Hivi Wafamasia wana nini?

Hivi Wafamasia wana nini?

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Hawa jamaa ndio wanaosimamia maduka ya dawa maarufu kama Pharmacy.

Jana nimeona wameungana na wanaharakati akina shangazi, kupinga agizo la mheshimiwa waziri Ummy, la kuondoa maduka ya dawa yaliyo karibu na Hospitali za umma kama inavyosema sheria yao wenyewe.

Sheria au kanuni ziliweka umbali wa maduka ya dawa na Hospitali,lakini pia umbali wa pharmacy na pharmacy bila kusahau umbali wa pharmacy na duka la dawa muhimu.

Lengo la sheria hizi lilikuwa kupeana nafasi za kufanya biashara. Kila mmoja mwenye pharmacy apate wateja.Pia lengo lilikuwa kuhakikisha huduma hii inasambaa sehemu nyingi ili kuwakaribia wananchi.

Sheria hii walitunga wao wenyewe,kupitia kwenye baraza lao wenyewe, na waliipitisha wao wenyewe kwa manufaa yao wenyewe kwani ililenga kulinda maslahi yao wenyewe.

Mfano ni pale wanapokataza duka la dawa muhimu lisiwepo mjini. Na waliwahi kujaribu kuyaondoa yote hata yaliyokuwepo tangu enzi za Mwinyi ili hawa wanaofungua sasa hivi wapate nafasi.

Kimsingi sheria hii haikuwa na umuhimu wowote pamoja na sababu walizozitoa.

Duka la dawa ni biashara, pamoja na kuwa ni huduma pia,wamiliki wana haki ya kuchagua eneo ambalo kwao wanadhani wataweza kufanya biashara hiyo kwa uzuri zaidi ili mradi wanazingatia sheria.

Leo ninawashangaa sana kwa kumgeuka waziri kana kwamba, amejitungia mwenyewe hizo sheria.

Wanajiweka kwenye kundi la watu wanaoonewa na wanasiasa, wakati sheria wametengeneza wao wenyewe. Huu si uungwana kabisa.
Mkilaumu, mlaumu baraza lenu la wafamasia, ambao kwa upande mwingine, wamekuwa wakilinda sasa maslahi yenu hata mnapovunja sheria,na siyo kumlaumu Ummy.

Kumbukeni ni huyu huyu Ummy, alitoa maagizo, wauguzi wote waondolewe pharmacy,ili wafamasia watumike katika kazi zao.

Alipokuja Gwajima, akasema ninyi ni wezi, hamuaminiki, hivyo akaendelea kuwa na wauguzi na wahudumu wa afya kwenye pharmacy za serikali. Hata ajira hakutoa za kutosha, licha ya vituo vya afya kuongezeka mara dufu. Huyo Gwajima ndiyo alikuwa rafiki yenu.

Mjisahihishe kwa kutumia akili zenu vizuri kumshauri waziri, na siyo kumpotosha hadi mnatunga sheria, halafu mnakuja kumgeuka
 
Sijaelewa mantiki ya hiyo sheria

Yaan mm nauza spare za gari uniambie nisikae karibu na garage kisa na wengine wapate wateja.

mbona hayo yatakuwa mateso kwa wateja yaan natoka na bibi yangu mgonjwa halafu tunaanza kukatiza mitaa tukiisaka dawa, c atanifia njian
 
Sijaelewa mantiki ya hiyo sheria

Yaan mm nauza spare za gari uniambie nisikae karibu na garage kisa na wengine wapate wateja.

mbona hayo yatakuwa mateso kwa wateja yaan natoka na bibi yangu mgonjwa halafu tunaanza kukatiza mitaa tukiisaka dawa..... C atanifia njian
Ni kama tu machinga kuhamishiwa kule porini, utadhani wanawauzia tembo na swala bidhaa zao.
 
Ndivyo hawa jamaa walivyofikiri,nashangaa leo wanalia wanaonewa,wakati walitengeneza sheria wao wenyewe
Sijaelewa mantiki ya hiyo sheria

Yaan mm nauza spare za gari uniambie nisikae karibu na garage kisa na wengine wapate wateja.

mbona hayo yatakuwa mateso kwa wateja yaan natoka na bibi yangu mgonjwa halafu tunaanza kukatiza mitaa tukiisaka dawa, c atanifia njian
 
Tatizo la Sekta ya Afya ni kuwa na watu wanoko. Madaktari, manesi mafamasia wote wanoko tu. Ni watu wanaopenda kujenga daraja hasa wakitaka wao kupita na wakishafika ng'ambo wanalibomoa ili wengine wasipite ati wanalinda profession zao. Hiki ulichoandika ni ukweli mtupu.
 
Hawa jamaa ndio wanaosimamia maduka ya dawa maarufu kama Pharmacy.

Jana nimeona wameungana na wanaharakati akina shangazi, kupinga agizo la mheshimiwa waziri Ummy, la kuondoa maduka ya dawa yaliyo karibu na Hospitali za umma kama inavyosema sheria yao wenyewe.

Sheria au kanuni ziliweka umbali wa maduka ya dawa na Hospitali,lakini pia umbali wa pharmacy na pharmacy bila kusahau umbali wa pharmacy na duka la dawa muhimu.

Lengo la sheria hizi lilikuwa kupeana nafasi za kufanya biashara. Kila mmoja mwenye pharmacy apate wateja.Pia lengo lilikuwa kuhakikisha huduma hii inasambaa sehemu nyingi ili kuwakaribia wananchi.

Sheria hii walitunga wao wenyewe,kupitia kwenye baraza lao wenyewe, na waliipitisha wao wenyewe kwa manufaa yao wenyewe kwani ililenga kulinda maslahi yao wenyewe.

Mfano ni pale wanapokataza duka la dawa muhimu lisiwepo mjini. Na waliwahi kujaribu kuyaondoa yote hata yaliyokuwepo tangu enzi za Mwinyi ili hawa wanaofungua sasa hivi wapate nafasi.

Kimsingi sheria hii haikuwa na umuhimu wowote pamoja na sababu walizozitoa.

Duka la dawa ni biashara, pamoja na kuwa ni huduma pia,wamiliki wana haki ya kuchagua eneo ambalo kwao wanadhani wataweza kufanya biashara hiyo kwa uzuri zaidi ili mradi wanazingatia sheria.

Leo ninawashangaa sana kwa kumgeuka waziri kana kwamba, amejitungia mwenyewe hizo sheria.

Wanajiweka kwenye kundi la watu wanaoonewa na wanasiasa, wakati sheria wametengeneza wao wenyewe. Huu si uungwana kabisa.
Mkilaumu, mlaumu baraza lenu la wafamasia, ambao kwa upande mwingine, wamekuwa wakilinda sasa maslahi yenu hata mnapovunja sheria,na siyo kumlaumu Ummy.

Kumbukeni ni huyu huyu Ummy, alitoa maagizo, wauguzi wote waondolewe pharmacy,ili wafamasia watumike katika kazi zao.

Alipokuja Gwajima, akasema ninyi ni wezi, hamuaminiki, hivyo akaendelea kuwa na wauguzi na wahudumu wa afya kwenye pharmacy za serikali. Hata ajira hakutoa za kutosha, licha ya vituo vya afya kuongezeka mara dufu. Huyo Gwajima ndiyo alikuwa rafiki yenu.

Mjisahihishe kwa kutumia akili zenu vizuri kumshauri waziri, na siyo kumpotosha hadi mnatunga sheria, halafu mnakuja kumgeuka
Hao wa phamasia wana monopoly ile mbaya ya kulinda masilahi yoa, mtu kupata cheti cha ufamasia sio mchezo hata kama umehitimu masoma paka na wenyewe wa kutungie mtihani na wa usahishe wenyewe ili kufuzu watu 200 wanafuzu wa tano au moja.........huo ujinga sijui kiongozi gani atakuja kuondoa huo udictrtor wa enzi za ujaama
 
Binafsi sioni tatizo kama wanajiwekea utaratibu wa kulinda taaluma yao,tatizo nililo nalo kwa hawa watu,ni kujitungia visheria vingi vya kijinga,vikianza kula kwao,wanasingizia watu wengine.

Mfano wao ndio wanamaduka ya dawa ya jumla ,na wateja wao ni hivi viduka vidogo vidogo.Lakini utakuta wanalalamika kuwa wezi wa dawa za serikali ni hawa wenye viduka vidogo.
Cha ajabu sasa,wanaosimamia vitengo vya dawa katika mahospitali ya serikali ni wao,wanao wauzia dawa haya maduka madogo kutoka maduka yao ya jumla ni wao, ila kesi ya wizi sio yao ila ni ya maduka madogo.
Waliowafundisha wauzaji na kuwapa kibali cha kuuza ni wao,wanaokagua maduka hayo ni wao,lakini wako mstari wa mbele kuja kwenye media kulaumu wanasiasa kwa kuruhusu maduka madogo.
Sasa yasipokuwepo,maduka yenu ya jumla mtamuuzia nani?
Je mnaweza kufungua maduka makubwa huku vijijii?
 
Waziri ameshasitisha Ile amri na amekiri ameelewa malalamiko yao Sasa sijui unajadili nini 🤷🤷🤷
 
Matanzania yana aina flani ya uchoyo hivi.........hayataki wengine wapate ndo ilivo!! kubaniana tuuuu...ukiangalia sana wafamasia wengi bibi zao au familia zao walikuwa wachawi!......au ni wachawi mpaka sasa...chunguza uone!
 
Back
Top Bottom