Hivi Wapenzi wa Muziki wa Congo DR hasa Masebene na Rhumba hapa JF hatuwezi kuja na huu Utaratibu?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kwa yoyote anayekutana na Miziki ya Sebene na Rhumba (ya zamani na mipya) awe anatuwekea hapa ili Wadau Wengine tujue na tuifuatilie na hata tuwe nayo?

Kama kuna Kitu GENTAMYCINE nakipenda na huwa Kinanifariji na kunifanya nijione sina Shida za Kimaisha wakati ninazo kuanzia Dar es Salaam hadi Kigoma ni Kusikiliza, Kuimba, Kutizama na Kucheza Nyimbo za Kikongo (Congo DR) tu.

Kwa mfano muda huu natizama Sebene Kali la Fally Ipupa ambapo mbele ya Video hii kuna Rhumba Kali sana la Wimbo mtamu wa Rhumba wa Associe natamani mno niweke hapa sema tu Bando langu halitoshi.

Kama kuna Mdau (Mpenzi wa Nyimbo za Congo DR hasa Misebene na Rhumba) hebu nenda YouTube kisha tafuta Tamasha la Fally Ipupa alilolifanya Mkoani Mwanza utaburudika mno hasa kuanzia dakika ya 34 na Sekunde 50 hadi dakika ya 58 na Sekunde 26.

Wakongo kwa Mziki tu Shikamooni.
 
Yani unasema kwa muziki tu kana kwamba hujui na kwenye ball ni hatari? hivi kuna Mtanzania wa kumfananisha na Mayele?
 
Ili hiyo Rhumba iendelee kukuburudisha kwa miaka 'alflela -ulela', mwambie huyo mtutsi mwenzio PK aache kuua na kupora huko Kivu. Kufanya hivyo ni 'ku destabilize' DRC na hiyo Rhumba unayoipenda itapotea.

Najiuliza hivi unavyowachukia DRC na kumtukuza PK, imekuwaje ukapenda muziki wao wa Rhumba?[emoji848]
 
Tafuteni Ngoma za JB Mpiana kama vile Omba, Feux de L'amour au Recto Verso ni Rhumba za hatari na hazichoshi.
 
 
Hawa jamaa ni nouma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…