Hivi wapo waliochomoka kimaisha kwa kutegemea mshahara wa chini ya million 1 tu?

Ukiweza kusave 65% ya mshahara wako kwa mwezi, basi kwa miaka mitatu au minne unaweza kuwa kwenye sehemu nzuri tu kimaisha...
 
biashara ni nzuri sana kuliko mshahara ila kama mtaji mdogo chukua vyote
 
MWINGI SANA HUO,MIMI NIPE LAKI NNE NA NUSU TU AFU UJE BAADA YA MIAKA MIWILI
 
Hapo mh kuna namna mbili kwanza unapo kuwa mtumishi ktk taasisi frani frani moja unatakiwa kujiongeza unapo pata haki yako ktk mwezi unatakiwa uwe na wazo ili uongeze kipato chako kama una pata laki 5,jibane tafuta vijana au kijana alafu wazo lako ktk mazingira uliopo ndo lifanye kazi ssa wakufanyie kazi uliyo waza hapo utaona unaongeza thamani ya haki yako ya mwezi.utajikuta ssa kwa mwezi unapata laki 5,ukijumlisha na ya wazo lako utapata laki 1,2,3..., na vijana umewalipa utakuwa una laki 6,7,8..... kwa mwezi ssa ukiendelea kwa mda wa mwaka mmoja unajiongeza kingine tena unajikuta ssa ukipiga hesabu hela unayolipwa na unayo ingiza ktk biashara ndipo unapo amua kuacha kazi ili ukasimamie miradi yako ndo maana utakuta watumishi wanaacha kazi wanajikita ktk biashara.mshahara laki 5 na biashara inaingiza kwa mwezi 1.2/1.5mill kipi bora sibora ukasimamia miradi yako ukiwaachia wasimamizi wanakuibia pesa inayo kalibia mshahara wako bora ukakabe ata wakiiba isiwe kubwa ya kukuumiza,wizi upo ilinawao wapate kuendesha maisha yao kiaina.
 
Ukiweza kusave 65% ya mshahara wako kwa mwezi, basi kwa miaka mitatu au minne unaweza kuwa kwenye sehemu nzuri tu kimaisha...
Nakubaliana na wewe kabisa ndugu yangu ukifanikiwa kusave 65% ya mshahara wako within 3 years unaweza kuwa sehemu nzuri ila sasa tukija kwenye uhalisia kwa maisha yetu asilimia kubwa ya watu wanakuwa wanakuwa tegemezi kwenye familia zao yani unashanga tu ukiukamata tu mshahara basi umeishia either kwenye kulipia madeni, ada ya mtoto au ndugu unaemsomesha, ujakaa vizuri kodi ujakaa vizuri tena unakutana na jambo lingine tena n.k ndio maana watu wanasema mshahara huwa hautoshi sasa jiulize maisha yanaendaje kama mshahara hautoshi? Mkuu ajira sio ya kutegemea kuendesha maisha tafuta kitu cha ziada cha kukuingizia pesa maana usipofanya hivyo sasa wahenga huwa nawasikia wanasema "FAINALI UZEENI".
 
Usave 65% ya mshahara kwa maisha gani? Acheni utani nyie
 
Hongera sasa tunafahamu kwamba una biashara.
 
Wapo,inategemea malengo na majukumu uliyo nayo.
Fedha ina tabia ya kujiongeza endapo inaangukia kwenye
mikono salama.

Wapo walioanza na kuku wawili
baadaye wanajikuta wana mabanda mengi ya kuku.
uchache au wingi wa fedha ya mshahara
wakati mwingine siyo kigezo kikuu cha kutoka kimaisha.
 
Usave 65% ya mshahara kwa maisha gani? Acheni utani nyie
Ndio nilikuwa namwambia jamaa hapo ni ngumu sana watu WACHACHE SANA ndio wanaweza hivyo ila kwa wengine ni impossible.
 
Mimi binafsi kipato changu kwa mwezi hakizidi laki 7 lakini kwa sasa namiliki nyumba ya kisasa na mwisho wa mwaka huu naagiza gari kwa ajili ya usafirishaji..kila kitu ni mipango na malengo...jitathimin na jielewe kidogo kina maana kuliko kikubwa
umefanikiwa kwa namna gani?
 


"dont depend on single source of income"
 
Wingi wa majukumu huwa ndio kikwazo na kuna baadhi ya hali unashindwa kuamua kipaumbele kiwe kipi ama uache kipi maana yote huwa muhimu na hapo ndipo kasheshe huanzia.
 
Ukiweza kusave hiyo 65% ya mshahara, basi familia yako itakuwa inajisaidia povu. Kwa mishahara hii ya laki 8? Save that amount, and you will end up spending it in hospital because of malnutrition.
 
Ukiwa kwenye uhalisia yaani umeajiriwa na una wanaokutegemea pokea laki tisa yako kwamwezi kisha wapeleke shule , matibabu, chakula , mavazi n.k mwenyewe utakuwa mwalimu wako mwenyewe kuwa inahitajika kujiongeza ,
sijakuelewa mkuu loading.........
 
sijakuelewa mkuu loading.........
Mkuu, inafikia hatua umepokea ka laki tisa, ukikaa tu kupiga mahesabu kote kameisha, na bado mahitaji ni mengi, watoto waende shule nzuri, sijui ujenge, ulee wazazi wako, navmengine mengi, hivi laki tisa itaonekana hapo?
Mwenyewe maisha yakufanya ujifunze, ujiongeze vipi hapo,
 
JIBU ndio. Uthibitisho, rejea watumishi wa umma kama Mtemi Endrew chenge, Nazir karamagi, Edward Lowassa, engineer Fredrick Sumaye, Dr kafumu, AG Wereme, AG mwanyika. Hawa wote wameishi kama watumishi wa umma na mawe waliyonayo hakuna wakuwagusa.
 
JIBU ndio. Uthibitisho, rejea watumishi wa umma kama Mtemi Endrew chenge, Nazir karamagi, Edward Lowassa, engineer Fredrick Sumaye, Dr kafumu, AG Wereme, AG mwanyika. Hawa wote wameishi kama watumishi wa umma na mawe waliyonayo hakuna wakuwagusa.
mhii si kweli, hawa ni majambawazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…