Hivi Warioba ametoa picha gani kwa watanzania?

Hivi Warioba ametoa picha gani kwa watanzania?

Mapambano Yetu

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
1,130
Reaction score
2,102
Warioba ni mwanasheria mzoefu hapa nchini. Si mgeni wa kanuni bungeni. Kinachonitatiza ni kitendo cha yeye kwenda kuhutubia bunge ilhali akifahamu wazi kuwa kanuni zinamhitaji rais aanze na Warioba amalizie. Hapa watanzania naona kama Warioba ana lake jambo.
 
Warioba ni mwanasheria mzoefu hapa nchini. Si mgeni wa kanuni bungeni. Kinachonitatiza ni kitendo cha yeye kwenda kuhutubia bunge ilhali akifahamu wazi kuwa kanuni zinamhitaji rais aanze na Warioba amalizie. Hapa watanzania naona kama Warioba ana lake jambo.
Kalazimishwa na wavunja kanuni,wawaza posho huku wakipiga meza ndiyooo ma ccm
 
Alikataa kuendelea kuhutubia baada ya Sitta kumwambia aendelee tu, na badala yake akaenda kukaa. Ametoa picha ya kwamba ni kweli hakupenda kuhutubia kabla ya Rais, na kwamba anaungana na wanaopinga Sitta kuvunja kanuni
 
Lakini ameonyesha msimamo pale alipoamuriwa na 6 aendelee kuwasilisha rasimu ila naye akagoma na kwenda kukaa
 
I hate politics, wanatumia muda mwingi kutafuta ujinga. Kwani bila ya katiba mpya hamuwezi kuishi?. Time wasting issue.
 
Alikataa kuendelea kuhutubia baada ya Sitta kumwambia aendelee tu, na badala yake akaenda kukaa. Ametoa picha ya kwamba ni kweli hakupenda kuhutubia kabla ya Rais, na kwamba anaungana na wanaopinga Sitta kuvunja kanuni

Angeonekana wa maana sana kama angekataa hata kuitikia wito au angeishia mlangoni bila kuingia ndani. Kuingia tu, amejishushia P.
 
Warioba ni mwanasheria mzoefu hapa nchini. Si mgeni wa kanuni bungeni. Kinachonitatiza ni kitendo cha yeye kwenda kuhutubia bunge ilhali akifahamu wazi kuwa kanuni zinamhitaji rais aanze na Warioba amalizie. Hapa watanzania naona kama Warioba ana lake jambo.

Katika hili Warioba hausiki kabisa. Yeye alifuata ualiko aliopewa kwa kuwa yeye siyo mjumbe wa bunge hilo. Yeye alialikwa na Mwenyekiti awasilishe rasimu ya pili. Kimsingi haikuwa kazi ya Warioba kumdai mwenyekiti afuate kanuni kwa kuwa kanuni hizo siyo yeye aliyeziweka na kama kuna kubadili kanuni yoyote ni jukumu la wabunge hao wa bunge la katiba na Mwenyekiti wake. Kwa hiyo kilichotokea anayepaswa kulaumiwa ni yule aliyemwalika Warioba awasilishe rasimu ya katiba leo. Tungemshangaa sana kama asingetokea bungeni tayari kuwasilisha rasimu kama ambavyo alitakiwa na viongozi wa bunge hilo. Kwa kutokea na kutoendelea tumeweza kuelewa kuwa Mwenyekiti alisigina kanuni. Huo ndio ukweli. Mzee Warioba amekutana na zahama za wajumbe hao kuvutana tu kwa mujibu wa kanuni. Samwel Sita alipaswa kutafsiri kanuni kama zilivyo. Na ni kweli alionywa mapema kufuata kanuni akajifanya kichwa ngumu.
 
Katika hili Warioba hausiki kabisa. Yeye alifuata ualiko aliopewa kwa kuwa yeye siyo mjumbe wa bunge hilo. Yeye alialikwa na Mwenyekiti awasilishe rasimu ya pili. Kimsingi haikuwa kazi ya Warioba kumdai mwenyekiti afuate kanuni kwa kuwa kanuni hizo siyo yeye aliyeziweka na kama kuna kubadili kanuni yoyote ni jukumu la wabunge hao wa bunge la katiba na Mwenyekiti wake. Kwa hiyo kilichotokea anayepaswa kulaumiwa ni yule aliyemwalika Warioba awasilishe rasimu ya katiba leo. Tungemshangaa sana kama asingetokea bungeni tayari kuwasilisha rasimu kama ambavyo alitakiwa na viongozi wa bunge hilo. Kwa kutokea na kutoendelea tumeweza kuelewa kuwa Mwenyekiti alisigina kanuni. Huo ndio ukweli. Mzee Warioba amekutana na zahama za wajumbe hao kuvutana tu kwa mujibu wa kanuni. Samwel Sita alipaswa kutafsiri kanuni kama zilivyo. Na ni kweli alionywa mapema kufuata kanuni akajifanya kichwa ngumu.

thanx sana. Hapa nimejifunza kitu.
 
Alikataa kuendelea kuhutubia baada ya Sitta kumwambia aendelee tu, na badala yake akaenda kukaa. Ametoa picha ya kwamba ni kweli hakupenda kuhutubia kabla ya Rais, na kwamba anaungana na wanaopinga Sitta kuvunja kanuni

Safi sana hiyo ndiyo misimamo tunayoitaka Sitta ni mtu mdogo sana kwa Warioba
 
Katika hili Warioba hausiki kabisa. Yeye alifuata ualiko aliopewa kwa kuwa yeye siyo mjumbe wa bunge hilo. Yeye alialikwa na Mwenyekiti awasilishe rasimu ya pili. Kimsingi haikuwa kazi ya Warioba kumdai mwenyekiti afuate kanuni kwa kuwa kanuni hizo siyo yeye aliyeziweka na kama kuna kubadili kanuni yoyote ni jukumu la wabunge hao wa bunge la katiba na Mwenyekiti wake. Kwa hiyo kilichotokea anayepaswa kulaumiwa ni yule aliyemwalika Warioba awasilishe rasimu ya katiba leo. Tungemshangaa sana kama asingetokea bungeni tayari kuwasilisha rasimu kama ambavyo alitakiwa na viongozi wa bunge hilo. Kwa kutokea na kutoendelea tumeweza kuelewa kuwa Mwenyekiti alisigina kanuni. Huo ndio ukweli. Mzee Warioba amekutana na zahama za wajumbe hao kuvutana tu kwa mujibu wa kanuni. Samwel Sita alipaswa kutafsiri kanuni kama zilivyo. Na ni kweli alionywa mapema kufuata kanuni akajifanya kichwa ngumu.

Mkuu ufafanuzi wako ni mzuri, kuna watu wanataka kupotosha kwa huu upuuzi wa Six.

Huu ujinga aulizwe Six kwa nini ameamua kuvunja kanuni zilizotungwa na wajumbe kwa zaid ya wiki mbili kwa Mamilioni ya walipakodi.!
 
Kumlaumu Warioba ni kutokumtendea haki.Kazi yake ni kukubali mwaliko tu,mambo ya kanuni hayamhusu.Ni sawa na padri ama shekh kazi yake ni kuongoza ibada,kama msikitini ama kanisani kuna muumini jambazi haimuhusu!
 
Ni wakati wa waTZ kuunganisha nguvu zetu kwa kuweka kando itikadi za vyama vya siasa kupinga aina yoyote ya uvurugajihuu
 
Katika hili Warioba hausiki kabisa. Yeye alifuata ualiko aliopewa kwa kuwa yeye siyo mjumbe wa bunge hilo. Yeye alialikwa na Mwenyekiti awasilishe rasimu ya pili. Kimsingi haikuwa kazi ya Warioba kumdai mwenyekiti afuate kanuni kwa kuwa kanuni hizo siyo yeye aliyeziweka na kama kuna kubadili kanuni yoyote ni jukumu la wabunge hao wa bunge la katiba na Mwenyekiti wake. Kwa hiyo kilichotokea anayepaswa kulaumiwa ni yule aliyemwalika Warioba awasilishe rasimu ya katiba leo. Tungemshangaa sana kama asingetokea bungeni tayari kuwasilisha rasimu kama ambavyo alitakiwa na viongozi wa bunge hilo. Kwa kutokea na kutoendelea tumeweza kuelewa kuwa Mwenyekiti alisigina kanuni. Huo ndio ukweli. Mzee Warioba amekutana na zahama za wajumbe hao kuvutana tu kwa mujibu wa kanuni. Samwel Sita alipaswa kutafsiri kanuni kama zilivyo. Na ni kweli alionywa mapema kufuata kanuni akajifanya kichwa ngumu.
Mkuu, umefafanua vema kabisa ila kuna watu sijui hufanya makusudi au ndo 'elimu' yetu ilivo kwa kweli inasikitisha mno.
 
Back
Top Bottom